Tuesday, October 07, 2008

Happy Birthday Mheshimiwa Rais

Rais Jakaya Mrisho Kikwete leo (Jumanne, Oktoba 7, 2008) ameadhimisha Siku yake ya kuzaliwa kwa kuhudhuria hafla fupi ya kushtukiziwa aliyoandaliwa na wafanyakazi wenzake wa Ikulu, Dar es Salaam.

Rais Kikwete amefikisha umri wa miaka 58 leo. Alizaliwa Oktoba 7, 1950 katika kijiji cha Msoga, Chalinze, Bagamoyo, Mkoa wa Pwani.

Katika halfa hiyo kwenye makazi yake rasmi, Rais Kikwete amepata nafasi ya kumsalimia binafsi kila mmoja wa wafanyakazi hao baada ya kuwa ameshiriki nao katika kuonja keki ya Siku hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya wafanyakazi hao katika halfa hiyo fupi, Katibu Mkuu wa Ikulu, Michael Mwanda amempongeza Rais Kikwete kwa kufikisha umri wa miaka 58 na kumtakia afya njema na maisha marefu.

Naye Rais amewashukuru wafanyakazi hao akisema kuwa utawala wake usingepata mafanikio yaliyopatikana bila kazi kubwa inayofanywa na wafanyakazi hao.

“Nawashukuruni sana kwa kunisaidia kwa kiasi kikubwa. Nawashukuruni pia kwa kuniandalia hafla hii fupi ya kushtukizia kwa sababu kama unavyojua sisi watu tuliozaliwa vijijini hatuna utamaduni wa namna hii wa kuadhimisha siku ya kuzaliwa ama kulishana keki.”

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

07 Oktoba, 2008

No comments:

NAIBU WAZIRI WA FEDHA AMWAKILISHA WAZIRI WA FEDHA KATIKA KONGAMANO LA 16 LA MWAKA LA WATAALAM WA UNUNUZI NA UGAVI – ARUSHA

Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Mhandisi Mshamu Ali Munde, amemwakilisha Waziri wa Fedha katika ufunguzi wa Kongamano la 16 la Mwaka la Wa...