Monday, July 31, 2017

TAMASHA LA ‘KOMAA CONCERT 2017’ LATIKISA DAR


Msanii wa Hip Hop, Chemical, akiwaburudisha mashabiki.
Ruby akifanya yake stejini
Mwana- FA naye akiwarusha vilivyo mashabiki wake.
Young D akifanya yake.
Dogo Aslay akikamua stejini.

TAMASHA la “KOMAA CONCERT 2017, la kituo cha redio cha Efm na TV-E jana lilifunika vilivyo katika viwanja vya Tanganyika Packers, Kawe, ambapo lilitawaliwa na burudani mbalimbali kutoka kwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya.
Komaa Concert’ linafanyika mara ya pili sasa baada ya kutikisa jijini Mwanza wiki zilizopita ambapo Mkoa wa Dar es Salaam lilifanyika jana.
Tamasha hilo lilitawaliwa na wasanii kama Dog Aslay, Mr. Blue,Young D, Msaga SumuShalo Mwamba na wengineo waliotoa burudani za kutosha kwa mashabiki wa muziki.
Vile vile, kulikuwa na mchezo wa bahati nasibu uliochezeshwa na kampuni ya BIKO ambao walikuwa wadhamini wakubwa wa tamasha hilo ambapo mshindi katika mchezo huo aliondoka na zawadi ya shilingi ya milioni kumikwa kutumia elfu moja tu kuchezea bahati nasibu hiyo.
Efm redio imekuwa ikifanya tamasha hilo kwa lengo la kuwashukuru wasikilizaji wake pamoja na kuendelea kuongeza masafa ya redio katika mikoa mbalimbali ya Tanzania.
NA HILALY DAUDI/GPL

No comments: