Wednesday, July 26, 2017

RC MAKONDA ATEMBELEA WODI MPYA YA KINA MAMA HOSPITALI YA AMANA JIJINI DAR ES SALAAM


 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Paul Makonda jana ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa wodi ya kisasa ya kinamama na watoto inayojengwa Hospital ya Amana yenye thamani ya shilingi Billion 1.2 ambapo ujenzi wake umekamilika kwa 100%.

Wodi hiyo ya kisasa itakuwa na uwezo wa kuchukuwa vitanda 150 ambapo ndani yake kutakuwa na Vifaa vya kisasa vya kutolea huduma, Vyumba vya Madaktari,vyoo vya kisasa,mabomba ya maji, taa za kisasa na sehemu ya kutosha ya wagonjwa kukaa wakati wakisubiri kuhudumiwa.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Paul Makonda akikagua maendeleo ya ujenzi kwenye moja ya chumba katika wodi ya kisasa ya kinamama na watoto inayojengwa Hospital ya Amana yenye thamani ya shilingi Billion 1.2 ambapo ujenzi wake umekamilika kwa 100%.

Wodi hiyo ya kisasa itakuwa na uwezo wa kuchukuwa vitanda 150 ambapo ndani yake kutakuwa na Vifaa vya kisasa vya kutolea huduma, Vyumba vya Madaktari,vyoo vya kisasa,mabomba ya maji, taa za kisasa na sehemu ya kutosha ya wagonjwa kukaa wakati wakisubiri kuhudumiwa.

 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Paul Makonda akizungumza na Wanahabari mara baada ya kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa wodi ya kisasa ya kinamama na watoto inayojengwa Hospital ya Amana yenye thamani ya shilingi Billion 1.2 ambapo ujenzi wake umekamilika kwa 100%.

Wodi hiyo ya kisasa itakuwa na uwezo wa kuchukuwa vitanda 150 ambapo ndani yake kutakuwa na Vifaa vya kisasa vya kutolea huduma, Vyumba vya Madaktari,vyoo vya kisasa,mabomba ya maji, taa za kisasa na sehemu ya kutosha ya wagonjwa kukaa wakati wakisubiri kuhudumiwa.

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Paul Makonda leo ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa wodi ya kisasa ya kinamama na watoto inayojengwa Hospital ya Amana yenye thamani ya shilingi Billion 1.2 ambapo ujenzi wake umekamilika kwa 100%.

Wodi hiyo ya kisasa itakuwa na uwezo wa kuchukuwa vitanda 150 ambapo ndani yake kutakuwa na Vifaa vya kisasa vya kutolea huduma, Vyumba vya Madaktari,vyoo vya kisasa,mabomba ya maji, taa za kisasa na sehemu ya kutosha ya wagonjwa kukaa wakati wakisubiri kuhudumiwa.

Ujenzi wa Wodi hiyo ni unafadhiliwa na Kampuni tanzu ya Mafuta na Saruji ya Amsons Group ambayo imekubali kumuunga mkono Mheshimiwa Makonda kwa kujenga wodi tatu wazazi na watoto kwenye Hospital za Amana, Temeke na Mwananyamala ambapo zote zitakuwa na uwezo wa kuchukuwa vitanda 450.

“Ujenzi huu na hatua iliyofikia inatoa matumaini mapya kwa kinamama, watoto na wakazi wa Dar es salaam juu ya upatikanaji wa huduma bora na nzuri kwenye Hospital zetu za Serikali,watu walishazoea huduma nzuri zinapatikana nje ya Hospital za Serikali lakini kwa sasa hali itabadilika, na nina uhakika ndani ya muda mfupi tutamuomba Rais Dr.Magufuli aje atuzindulie hizi wodi kama ishara ya kumbukumbu ya kazi aliyoianza alipotembelea Hospital ya Muhimbili na kukuta watu wamelala chini na kutafuta majibu, sisi wasaidizi wake ametupa kazi ya kutatua kero za wananchi, hivi ndivyo tunavyozitatua kwa vitendo” Alisema.

Aidha Makonda amesema wodi hiyo itazidisha upatikanaji mzuri wa huduma bora za Afya kwa wakazi wa jiji la Dar es salaam huku akieleza kuwa lengo lake ni kuhakikisha Dar es Salaam inakuwa mkoa unaotoa huduma bora za Afya.

“Kama mnakumbuka wakati tunakuja wodi iliyokuwa ikitumik akinamama walikuwa wakilundikana chini na wengine wanatumia kitanda kimoja zaidi ya watatu hadi wanne na wakati mwingine walikuwa wakilazimika kurudi nyumbani kabla ya muda wa madaktari kuruhusu kutokana na mazingira duni yaliyokuwa yakikabili wodi hiyo, lakini wodi hii itamaliza kero hiyo” Aliongeza Makonda.

Hata hivyo Makonda amewataka wadau wa maendeleo wenye dhamira ya kuchangia shughuli za Maendeleo kwenye Mkoa wa Dar es salaam kujitokeza kwa wingi Ofisini kwake na Ofisi za Wilaya kuungana na Serikali kuujenga Mkoa huo.

“Nawapongeza watumishi na wafanyakazi wa Afya kwenye Hospital za Amana, Temeke na Mwananyamala kwa kazi kubwa wanayoifanya kupunguza kero kwenye Sekta ya Afya” Alisema Makonda.

No comments: