Wednesday, July 26, 2017

BALOZI WA KUWAIT NCHINI JASEM AL-NAJEM AUNGA MKONO SERA YA MAGUFULI YA ELIMU BURE


Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mhe. Filberto Sanga akizunguma na wanacnhi wa kijiji cha Mpafu katika hafala ya uzidunzi wa visima vitano vyenye thamani ya zaidi ya milioni hamsini vilivyotolewa msaada na ubalozi wa Kuwait nchini Visima hivyo vitano vilivyozinduliwa vimejengwa katika vijiji vya Kisayani, Kerekese, Mpafu, Sotele na Sangasanga 
Balozi wa Kuwait nchini, Mhe Jaseem Al Najem akizungumza na wanchi wa kijiji cha Mpafu kataika uzinduzi wa visima virefu vitano vilivyo fadhiliwa na Ubalozo wa Kuwet nchini leo mkoani Pwani.
Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Abdalah ulega akimshukuru Balozi wa Kuwait nchini, Mhe. Jaseem Al Najem kwakuchimba visima hivyo.
Mganga Mkuu Wilaya ya Mkuranga Dkt.Steven Mwandambo wa (kwanza kushoto) akitoa maelekezo mbele ya Balozi wa Kuwait nchini, Mhe Jaseem Al Najem,watendaji wakuu wa wilaya katika hafla ya uzidunzi wa visima virefu vitano vilivyo vyenye thamani ya zaidi ya milioni hamsini.
Balozi wa Kuwait nchini, Mhe Jaseem Al Najem wa (pili kushoto) akikabidhi watendaji wa wilaya ya mkuranga mabeseni hamsini pamoja na vifaa vya akina mama wakati wa kujifungua katika hospital ya wilaya hiyo.Picha zote na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii
Balozi wa Kuwait nchini, Mhe Jaseem Al Najem akizindua kisima katika kijiji cha Mpafu kwa kushirikiana na Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga,Filberto Sanga, Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Abdalah ulega.
Picha ya pamoja
Balozi wa Kuwait nchini, Mhe Jaseem Al Najem wakionja maji baada ya kuzindua kisima katika kijiji cha Mpafu kwa kushirikiana na Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga,Filberto Sanga, Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Abdallah ulega.Picha na habari na Emmanuel Massaka wa Globu ya Jamii.

Halmashauri ya wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani imezindua visima vitano virefu vyenye thamani ya zaidi ya milioni hamsini vilivyotolewa msaada na ubalozi wa Kuwait nchini.

Visima hivyo vitano vilivyozinduliwa vimejengwa katika kijiji cha Kisayani, Kerekese, Mpafu, Sotele na Sangasanga vya Mkuranga.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo wilayani mkuranga mkoani pwani balozi wa Kuwait Mhe. Jasem Al-Najem alisema serikali ya Kuwait kupitia ubalozi uliyopo nchini inafanya jitihada kubwa kusaidia Tanzania katika nyanja mbalimbali zinazohusu Jamii ikiwemo afya pamoja na maji.

Aidha balozi Jasem alisema katika kuunga mkono sera ya Rais wa awamu ya tano Dkt John Pombe Magufuli ya elimu bure wameamua kuanzisha mradi ujulilanao wa kisima kila shule ili kupinguza changamoto ya maji pamoja na kuakikisha wanafunzi wanapata maji safi na salama kwa wakati lengo nikuboresha elimu nchini."maji no muhimu sana uchimbaji wa maji mashuleni sio utasaidia wanafunzi na wanachi wanaoishi karibu na kusaidia kwa kiasi kikubwa wanafunzi kupata huduma kamili ya masomo"alisema.

Pia ubalozi huo umetoa mabeseni hamsini pamoja na vifaa vya akina mama wakati wa kujifungua katika hospital ya wilaya ya mkuranga ili kuboresha huduma ya afya.

Aidha Mbunge wa viti maalum mkoa wa pwani Zainabu Vulu alisema afya ya Mama na mtoto ni muhimu sana na kukikosekana vifaa afya ya mama itakuwa hatarishi."tunashukuru sana kwa msaada wenu huu utasaidia sana mama kujifungua mtoto mwenye afya na mwenyewe kubaki mwenye afya "alisema.

Hata hivyo Mbunge wa jimbo la mkuranga mh. Abdalah Hamis Ulega amewashuru kuwait kwa msaada huo na kusema mpaka sasa wameshachimba visima ishirini visima nane kati ya hivyo ni vya serikali.

Aidha aliongeza kama Mbunge wa mkuranga aliguswa na kuamua kutafuta wafadhili baada ya kupata barua kutoka kwa Mwalimu mkuu wa shule ya msingi kisayani kutaka kuifunga shule hiyo kutokana na changamoto ya maji,ndipo akawatafuta wafadhili hao ambao wamechima visima virefu vitano vya maji wilayani humo.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya mkuranga Filiberto Sanga alitoa wito kwa wanachi kuhakikisha wanakitunza kisima hicho kisiharibike.

No comments: