Saturday, September 13, 2008

Wapambanaji wapata ajali

Herry Makange (kushoto) na Athuman Hamisi.

Herry Makange akimsaidia Athumani mara baada ya kumtoa katika gari



Gari ambalo alikuwa akisafiria Athumani Hamisi, Hery Makange na Anthony Siame namba T 961 AGT baada ya kupata ajali.
Wapigapicha za Habari wa tatu wa vyombo vya habari jijini Dar es salaam leo wamenusurika kufa katika ajali ya gari iliyotokea asubuhi wakiwa njiani kelekea Kilwa katika futari maalum iliyoandaliwa na kampuni ya Vodacom kupitia Voda Foundation.
Wapigapicha hao ni Athumani Hamisi wa Daily News na Habarileo, Herry Makange wa DTV na Channel 10 pamoja na Anthony Siame wa New Habari Cooperation.

Halizao zinaendelea vyema isipokuwa Athumani aliyepata majeraha kichwani tumboni na mkononi baada ya gari alilokuwa akiendesha kupinduka mara kadhaa kabla ya kutua nje ya barabada.
Athumani amesema walikuwa katika mwenzo wa kawaida na walipokaribia Kibiti sehemu ambako barabara ina changarawe juu ya lami, gari iliyumba na kuserereka na kuanguka.
Globu hii ya jamii inamuombea mpiganaji huyu apate nafuu ya haraka. Pia inatoa shukrani kwa msaada wa hali na mali ambayo Vodacom inatoa kwa majeruhi, pia asante ziende kwa Ruge Mutahaba wa Clouds FM ambaye alihakikisha gari inavutwa hadi Dar ambako imeegeshwa kituo kikuu cha kati cha polisi.
Vile vile shukrani za pakee ziwaendee pia Herry Makange aliyebaki kulinda gari na vifaa vya kazi ambavyo vyote vipo salama, na Anthony Siame ambaye hakubanduka ubavuni pa Athumani hadi anafika Muhimbili.
Picha zilipigwa na Siame, na hiyo ya hospitali ilipigwa na bernard rwebangira na pia zipo katika
mrokim.blogspot.com na issamichuzi.blogspot.com na haki-hakingowi.blogspot.com

No comments: