Wednesday, September 10, 2008

Maamuzi mazito CCM




HATIMA ya mwanasiasa kijana, Nape Nnauye na jina la mgombea wa ubunge ya jimbo la Tarime Mjini ndio mambo yanayotarajiwa kukuna vichwa vya wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) baada ya vichwa 39 vya Kamati Kuu kujadili jana hadi usiku wa manane.

Hakuna uamuzi uliotangazwa jana baada ya Kamati Kuu, chini ya uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete, kujadili masuala hayo, pamoja na agenda nyingine za NEC kwa vipindi viwili, cha kwanza kikianza saa 9.00 alasiri na kingine saa kikianza saa 3:00 usiku.
“Wameamua kupumzika kwa ajili ya futari na tumeambiwa kuwa watakutana tena saa 3:00 usiku kuendelea na kikao cha maandalizi ya NEC,” alisema mmoja wa wafanyakazi kwenye jengo la CCM Makao Makuu mjini Dodoma.

Rais Jakaya Kikwete aliwasili Dodoma jana mchana na aliingia kwenye chumba cha mkutano, akiwa na lundo la nyaraka, hali iliyoonyesha kuwa kikao hicho kilikuwa na shughuli kubwa ya kujadili kabla ya kuyasukumia masuala hayo moto kwenye kikao cha leo.

No comments: