UAMUZI wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UV-CCM) wa kumvua uanachama Nape Moses Nnauye, sasa unaonekana dhahiri kukitikisa chama kizima.
Mtikisiko huo umedhihirika kufuatia kauli za wazi za kutoridhishwa na kustushwa na uamuzi huo wa Baraza Kuu, ambazo zimetolewa na makada waandamizi wa chama hicho, wakiwemo Mawaziri Wakuu wawili wastaafu Cleopa David Msuya na Frederick Sumaye.
Licha ya kauli hizo za wazi za makada hao waandamizi, taarifa kutoka ndani ya Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC) ya chama hicho, hadi jana bado ilikuwa ikitambua nafasi za Nape, ambaye ni mwana wa aliyekuwa kada mwandamizi wa CCM marehemu Brigedie Moses Nnauye.
Kauli mpya ya Katibu Mkuu Yusuph Makamba, kwamba Nape bado atabaki na nafasi zake ndani ya chama ni ishara pia kwamba, chama ikiwemo CC na NEC hazijabariki maamuzi ya Baraza Kuu la UV-CCM.
Wednesday, September 10, 2008
Pigo la kwanza kwa Makamba
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
NHC YAKABIDHI MSAADA KWA WATU WENYE ULEMAVU UBUNGO
Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), kupitia kwa Afisa wake Mkuu wa Habari, Yahya Charahani, limekabidhi msaada wa vifaa vya kusaidia watu we...

-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
Mwanamuziki toka Jamhuri ya KIdemokrasia ya Kongo, Mbilia Bel akitumbuiza katika viwanja vya bunge mjini Dodoma jana. Picha na Jube Tranquil...
-
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA ...
No comments:
Post a Comment