UAMUZI wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UV-CCM) wa kumvua uanachama Nape Moses Nnauye, sasa unaonekana dhahiri kukitikisa chama kizima.
Mtikisiko huo umedhihirika kufuatia kauli za wazi za kutoridhishwa na kustushwa na uamuzi huo wa Baraza Kuu, ambazo zimetolewa na makada waandamizi wa chama hicho, wakiwemo Mawaziri Wakuu wawili wastaafu Cleopa David Msuya na Frederick Sumaye.
Licha ya kauli hizo za wazi za makada hao waandamizi, taarifa kutoka ndani ya Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC) ya chama hicho, hadi jana bado ilikuwa ikitambua nafasi za Nape, ambaye ni mwana wa aliyekuwa kada mwandamizi wa CCM marehemu Brigedie Moses Nnauye.
Kauli mpya ya Katibu Mkuu Yusuph Makamba, kwamba Nape bado atabaki na nafasi zake ndani ya chama ni ishara pia kwamba, chama ikiwemo CC na NEC hazijabariki maamuzi ya Baraza Kuu la UV-CCM.
Wednesday, September 10, 2008
Pigo la kwanza kwa Makamba
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
RAIS SAMlA AFANYA MAZUNGUMZO NA MJUMBE MAALUM WA RAIS TSHISEKEDI
Dar es Salaam, 26 Machi 2025 – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan , amekutana na kufanya mazungu...
-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
(Picha na Yahya Charahani) Kwa wale waliokulia maeneo haya, hili ni jambo la kawaida ukitoka mjini, shambani sijui hadi wapi kote ni haya h...
-
NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2014 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA ...
No comments:
Post a Comment