UAMUZI wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UV-CCM) wa kumvua uanachama Nape Moses Nnauye, sasa unaonekana dhahiri kukitikisa chama kizima.
Mtikisiko huo umedhihirika kufuatia kauli za wazi za kutoridhishwa na kustushwa na uamuzi huo wa Baraza Kuu, ambazo zimetolewa na makada waandamizi wa chama hicho, wakiwemo Mawaziri Wakuu wawili wastaafu Cleopa David Msuya na Frederick Sumaye.
Licha ya kauli hizo za wazi za makada hao waandamizi, taarifa kutoka ndani ya Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC) ya chama hicho, hadi jana bado ilikuwa ikitambua nafasi za Nape, ambaye ni mwana wa aliyekuwa kada mwandamizi wa CCM marehemu Brigedie Moses Nnauye.
Kauli mpya ya Katibu Mkuu Yusuph Makamba, kwamba Nape bado atabaki na nafasi zake ndani ya chama ni ishara pia kwamba, chama ikiwemo CC na NEC hazijabariki maamuzi ya Baraza Kuu la UV-CCM.
Wednesday, September 10, 2008
Pigo la kwanza kwa Makamba
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA BELARUS AWASILI NCHINI KWA ZIARA YA KIKAZI
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Belarus, Mheshimiwa Maxim Ryzhenkov, amewasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia Aprili...
-
Hapa mmoja wa watoto hao akiwa na kijana mwenzake mwenye miaka 18, wote wako sawa lakini yeye hawezi kuzungumza kama watu wa kawaida. Mama S...
-
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu na timu ya Wakurugenzi wa Shirika la Nyumba la Taifa akiwa katika ...
-
Pascal Mayalla akiwa katika chumba cha wagonjwa Daraja la kwanza katika hospitali ya mkoa wa Dodoma ambako amelazwa kwa matibabu baada ya ku...
No comments:
Post a Comment