Monday, June 30, 2014

SHEREHE ZA KUAGA WASTAAFU WA JESHI LA MAGEREZA MKOANI MWANZA ZAFANA JIJINI MWANZA


  Aliyekuwa Mkuu wa Magereza Mkoani Mwanza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza Mstaafu, Raphael Mollel akitoa nasaha zake kwa niaba ya Wastaafu wote wa Jeshi la Magereza Mkoani Mwanza katika sherehe za kuwaaga Wastaafu wa Magereza Mkoani Mwanza.
  Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja akitoa hotuba fupi kwa Maofisa wa Jeshi la Magereza na Wageni Waalikwa (hawapo pichani) katika Sherehe za kuwaaga Wastaafu wa Jeshi la Magereza Mkoani Mwanza.
  Wageni Waalikwa katika sherehe za kuwaaga Wastaafu wa Jeshi la Magereza Mkoani Mwanza wakitosi vinywaji na Meza Kuu kama inavyoonekana katika picha.
  Meza Kuu katika sherehe za kuwaaga Wastaafu wa Jeshi la Magereza Mkoani Mwanza (katikati) ni Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza Nchini, John Casmir Minja ambaye pia ndiye aliyekuwa Mgeni rasmi katika sherehe hizo zilizofana katika Ukumbi wa Gereza Kuu Butimba, Mwanza.
  Maafisa na Askari wa Magereza Mkoani Mwanza wakimsikiliza Mgeni rasmi Kamishna Jenerali wa Magereza, John Casmir Minja(hayupo pichani) wakati akitoa hotuba yake fupi katika sherehe za kuwaaga Wastaafu wa Jeshi la Magereza Mkoani Mwanza katika Ukumbi wa Bwalo la Gereza Kuu Butimba, Jijini Mwanza.

No comments: