Thursday, June 26, 2014

MAKAMU WA RAIS WA CHINA ATEMBELEA SHIRIKA LA RELI LA TANZANIA NA ZAMBIA (TAZARA)

PIX 1 (2)PIX 2 (2)Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Li Yuanchao (kulia) akiangalia jengo la Makao Makuu ya Ofisi ya Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA) mara baada ya kuwasili Makao Makuu ya shirika hilo leo jijini Dar es Salaam kwenda kuangalia miundo mbinu ikiwemo mabehewa na injini za treni za shirika hilo.
PIX 4 (2)Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Li Yuanchao (kushoto) akiangalia ramani ambayo reli ya TAZARA inapita kuanzia kituo cha Dar es Salaam wakati alipotembelea Makao Makuu ya Shirika la Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA) jana jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuangalia miundo mbinu ikiwemo mabehewa na injini za treni za shirika hilo. Kulia ni Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Harrison Mwakyembe.
PIX 7 (1)Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Harrison Mwakyembe akishuka toka ndani ya treni ya abiria ya TAZARA kuelekea katika kituo cha mizigo cha TAZARA kilichopo mtaa wa Yombo jijini Dar es Salaam.
PIX 8 (1)Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Li Yuanchao akishuka toka ndani ya treni ya abiria ya TAZARA kuelekea katika kituo cha mizigo cha TAZARA kilichopo mtaa wa Yombo jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kupatiwa maelezo ya kina kuhusiana na reli hiyo.
PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-MAELEZO.

No comments: