Friday, November 23, 2012

MBEKI MGENI RASMI MAJADILIANO YA UONGOZI AFRIKA DAR ES SALAAM

 Rais Mstaafu wa awamu ya pili ya utawala huru wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki (kulia) akifafania jambo wakati wa Majadiliano ya duara kuzungumzia uongozi barani Afrika na changamoto za maendeleo uliofanyika jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mwenyekiti wa Mdahalo huo ulioandaliwa na Taasisi ya UONGOZI Tanzania, Waziri Mkuu Mstaafu, Cleopa David Msuya. Mbeki alikuwa Mgeni Rasmi katika mdahalo huo.
 Mwenyekiti wa Majadiliano ya duara kuzungumzia uongozi barani Afrika na changamoto za maendeleo, ulioandaliwa na Taasisi ya UONGOZI Tanzania, Waziri Mkuu Mstaafu, Cleopa David Msuya akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mdahalo huo jijini Dar es Salaam.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Prof. Joseph Semboja, akizungumza katika mdahalo huo.
 Rais Mstaafu wa awamu ya pili ya utawala huru wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki (kulia) akikiwa mwenye tabasamu wakati Mwenyekiti wa Majadiliano ya duara kuzungumzia uongozi barani Afrika na changamoto za maendeleo ulioandaliwa na Taasisi ya UONGOZI Tanzania, Waziri Mkuu Mstaafu, Cleopa David Msuya akitoa ufafanuzi wa majadiliano.
 waziri Mkuu Mstaafu, Cleopa David Msuya na Mwenyekiti wa Mdahalo wa Uongozi Afrika, pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Prof. Joseph Semboja (katikati) wakimsikiliza Balozi wa kwanza wa Tanzania nchini Afrika Kusini Ami Mpungwe ambaye kwa sasa ni mfanyabiashara na Mwenyekiti wa Tanzanite One muda mfupi kabla ya kuwasili kwa Mgemi rasmi wa Majadiliano ya duara kuzungumzia uongozi barani Afrika na changamoto za maendeleo. 
Mawaziri Wakuu Wastaafu wa Tanzania, Cleo David Msuya (kulia)  na Salim Ahmed Salim wakijadiliana jambo muda mfupi kabla ya kuanza Majadiliano ya duara kuzungumzia uongozi barani Afrika na changamoto za maendeleo.
 
 Rais Mstaafu wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki, (Kulia), akimtania Waziri Mkuu Mstaafu na mwenyekiti wa Tume ya mabadiliko ya katiba ya Tanzania, Joseph Warioba, wakati marafiki hao walipokutana kwenye majadiliano ya duara kuzungumzia uongozi barani Afrika. 
 Waalikwa mbalimbali wakiwa katika chumba cha majadiliano.
 Naibu waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Januari Makamba, akichangia mada katika majadiliano hayo ya Duara. Makamba alizungumzia sana kuhusu masulala ya uchumi.
 Mmoja wa waalikwa akichangia mada
 Mwenyekiti wa Shirikisho la Wenye Viwanda Tanzania (CTI) Bw. Felix Mosha akizungumza.
 Meza kuu ikifuatilia kwa ukaribu majadiliano hayo. kutoka kushoto ni Rais Mstaafu wa afrika Kusini, Thabo Mbeki, Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Prof. Joseph Semboja na Mdhamini wa taasisi ya Thabo Mbeki, Gloria.
Arnod Kileo nae akichangia mada, kulia ni Prof. Toli Mbwete, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria Tanzania, ni ofisa kutoka Bank M.
Mwenyekiti wa Majadiliano ya duara kuzungumzia uongozi barani Afrika na changamoto za maendeleo ulioandaliwa na Taasisi ya UONGOZI Tanzania, Waziri Mkuu Mstaafu, Cleopa David Msuya akitoa ufafanuzi wa majadiliano.Kulia ni Mgeni Rasmi, Rais Mstaafu wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki.
 Waziri wa mambo ya Nje, Bernard Membe (kulia), waziri Makuu Mstaafu, Cleopa Msuya na Rais Mstaafu wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki wakifuatilia Majadiliano ya duara kuzungumzia uongozi barani Afrikajijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya waalikwa wakiwemo wahariri wa vyombo vya habari walihudhuria majadiliano hayo. kushoto ni Gabi Mgaya kutoka Daily News.
 Mwongozaji wa Majadiano hayo, Sauda Simba Kilumanga akisema jambo muda mfupi kabla ya kufunga.
Rais Mstaafu wa Afrika Kusini, Thabo Mbeki akizungumza jambo na Waziri Mkuu Mstaafu, na Mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Sinde Warioba huku Katikati waziri wa Mambo ya nje na Ushirikaino wa Kimataifa, Bernard Membe akichangia wakati viongozi hao wakitoka katika Majadiliano ya duara kuzungumzia uongozi barani Afrikayaliyoandaliwa na Taasisi ya UONGOZI jijini Dar es Salaam.

No comments: