Monday, June 17, 2013

SOMA TAMKO RASMI LA CHADEMA KWA WANANCHI JUU YA KINACHOENDELEA KWENYE CHAGUZI NDOGO ZA MARUDIO KWA KATA MBALIMBALI NCHINI


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinatoa taarifa za Hujuma zinazoendelea katika chaguzi za marudio kwa kata mbalimbali hapa nchini.
Kwa masikitiko makubwa CHADEMA kinatoa taarifa ya matukio ya kusikitisha yanayoendelea katika chaguzi hizi,kama ifuatavyo;

1. KATA YA IYELA,MBEYA.

Katika kata hii Gari la Chama Cha Mapinduzi lenye Usajili namba T 704 BEU,likiwa na watu wawili wanaotambulika kwa majina ya Moris na Nosy,waliwateka vijana wa CHADEMA na mmoja wao kuchomwa kisu,aliechomwa kisu anaitwa Meshack Bernard.Vijana wa CCM waliokamatwa wameachiwa huru na jeshi la polisi na sasa wanatumia gari nyingine yenye rangi nyekundu Toyata Surf namba T-173 ANE,wakiendelea kufanya vitendo hivo viovu.

Na katika kituo cha kupigia kura cha SIDO ,vituo 3 vimelundikwa sehemu moja na eneo hilo kuna Karakana ambayo inawafanya watu kuingia na kutoka kinyume na sheria za uchaguzi.

2. KATA YA MBALAMAZIWA ,MUFINDI KASKAZINI.
Watu sita wamepigwa kwa marungu na visu na kuumizwa vibaya muda huu.Idadi ya vitisho katika kata hii ni kubwa mno hali iliyopelekea idadi ndogo ya watu kujitokeza kupiga kura.

4. NYAMPU LUKANO, SENGEREMA 

Viongozi na makada wa CCM waligawa mapanga kwa vijana wao na kukata watu.Vijana 3 wa CHADEMA wamechomwa kisu na kujeruhiwa vibaya sana.

5:KATA YA MINEPA,MOROGORO.

Tukio lililotokea huko ni kuchomwa moto PIKIPIKI mali ya Chama(M4C) na vijana wa CCM(greenguard). Vile vile Katibu wa Chama wilaya ndugu Lucas Daniel amepigwa na kuumizwa na mwenzake amekatwa vidole.

3.KATA YA MANCHIRA,SERENGETI-MARA
Tumepokea taarifa kuwa Mkuu wa Wilaya kujihusisha na vitendo vya utoaji rushwa kwa wapiga kura,kwa lengo la kuwezesha CCM kushinda. Vijana wetu ni mashuhuda wa tukio hilo na wako tayari kutoa ushahidi juu ya hili piai wameshuhudia vijana wa CCM wakiwa na Bastola na baadhi yao kukamatwa na vijana wa CHADEMA na kupelekwa polisi

Hali kadhalika Jeshi la Polisi limekamata vijana wetu kuanzia jana jioni hadi leo hii na wamekuwa wakitumia mabomu na hivyo kuwajeruhi.Kuna vijana ambao wametekwa na hawajulikani walipo na majina yao na wanakotoka ni kama ifuatavyo
-Barena Maro-Bwitengi
-Samson Ogao-Rwamchanga
-Adam Samson-Bwitengi
-Emmanuel Eliya-Bwitengi
-Onyango Otaro-Miseke
-Manginare Samson-Miseke
-Elija Wilson-Miseke
-Banage Nanai-Rwamchanga
-Matororo saina-Rwamchanga
-Pikipiki Simba-Rwamchanga
John Oninga-Rwamchanga

Na baadhi ya gari zifuatazo zilikua zikishiriki opereshani ya kuwateka wafuasi wa CHADEMA magari hayo ni yenye namba zifuatazo za usajili T286 BFB, T545BFE zote Landcruiser za CCM na T352 AHD.
Diwani wa CHADEMA kata ya MUGUMU Mh.Marwa Waryoba amekamatwa na polisi yupo kituoni ili kumyima fursa ya kukugua zoezi la upigaji kura kama sheria inavyomtaka.

3. KATA YA MIANZINI,DAR ES SALAAM.
Tukio lililotokea huko ni kutekwa kwa wanachama na kiongozi wa Chama. Watu hawa walitekwa na kufungwa vitambaa vyeusi machoni,kisha kupigwa na kuumizwa vibaya. Mmoja kati ya vijana hao ni Katibu wa Vijana CHADEMA tawi la machinjioni anaeitwa Julius Vedastua na mpaka sasa yuko hospital.
Tukio lingine linaloendelea katika kata hii ni vitendo vya Rushwa,makada wa CCM wamekuwa wakivuta watu kutoka kwenye mistari na kuwapatia pesa.
Hali kadhalika kwa baadhi ya maeneo katika kata hii ni kuwa na wasimamizi wengi katika kituo kimoja,na wasimamizi hao wamekuwa wakiwaongoza watu kupiga kura mpaka kwenye ile sehemu ya kupigia kura na kuwapa maelezo juu ya nani wa kumchagua,kitendo ambacho ni kinyume na Sheria.

KATA YA STESHENI, NACHINGEA,LINDI.
Taarifa tulizonazo zinasema kuwa Magari ya CCM yamekuwa yakisomba wapiga kura na kati ya magari yanayotumika ni gari lenye usajili namba T670 DEU.

KATA YA DONGOBESH,MANYARA.
Katika kata hiyo,makada wa CCM wanawavamia katika vilabu vya pombe na kuwanunulia wananchi pombe kama hongo ya kutaka kupigiwa kura,na baada ya kuwanunulia pombe wamekuwa wakiwasomba kwa magari na kuwapeleka katika vituo vyao vya kupigia kura,kitendo hichi ambacho ni kinyume na sheria.

KATA YA GENGE,TANGA.
Matukio yaliyotokea huko ni vijana wa CCM kuwakamata vijana wetu wa Red Brigade na kuwapiga na kuwaumiza. Tukio hili limesharipotiwa polisi.

KATA YA MAKUYUNI,ARUSHA.
Vijana wa Kimasai ambao wamekodiwa na Chama cha Mapinduzi wamekuwa wakivamia wanachama na viongozi wetu na kuwapiga,katika kata hii ndio tukio la kumpiga na kumjeruhi Mh Mbunge Joshua Nasari limefanyika.

Aidha kuhusu mauaji ya Arusha Mwenyekiti wa Chama Taifa,Mh Freeman Mbowe ameshatoa


msimamo wa chama juu ya tukio hilo.


Imetolewa na :

Erasto Tumbo(Afisa Mwandamizi Uenezi)

No comments: