Sunday, June 16, 2013

MIAKA 13 YA LADY JAYDEE 'ANAKONDA' NI FUNIKA MBAYA

 Mwana dada nguli katika Sanaa ya Muziki nchini Tanzania na Mshindi wa Tuzo ya Mwanamuziki bora wa kike mara kadhaa na mwaka huu, Judith Wambura a.k.a Lady JayDee a.k.a Jide a.k.a Mama somefood a.k.a Komando hatimaye usiku wa kumakia jana alifanya show yake kali ya kutimiza miaka 13 katika sanaa ya Muziki nchini.

Show hiyo kali na ya aina yake ambayo awali ilikuwa ifanyike Mei 31, mwaka huu katika ukumbi wa Nyumbani Lounge Kinondoni jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha Msanii mwenzake Albert Mangwea ilifanyika jana licha ya kuwa palitokea msiba wa msanii mwingine Langa.

Jide ambaye alisindikizwa na wasanii kibao akiwepo Mkongwe Hamza Kalala, Prof. J, Mbunge wa Mbeya Mjini ambaye ni Mkongwe katika mziki wa Kizazi kipya Joseph Mbilinyi 'Sugu', Juma Nature na wengine wengi.

Watu wakiwa wamefurika kiasi cha kukosa kupenyeza mguu Lady JayDee alitumbuiza jukwaani kwa nyimbo zake kadhaa za zamani ambazo zilionesha kukonga vilivyo nyoyo za mashabiki na wapenzi wake ambao sasa anawapeleka kwa staili ya Nyoka Mkali ANACONDA.


 Sugu akiwa jukwaani
 Sir Juma Nature akimtambulisha M to the P ambaye nae alikuwepo ukumbini hapo.
 Hii ndio Wanaumeeeee....!!!
Mambo ya Anaconda haya ...yalikuwepo live.
 Mashabiki wakifuatilia show hiyo...
 Hii ni burudani kwa staili ya Anaconda...
 Christina Manongi 'Sinta' akifurahia burudani kali katika onesho hilo la Lady JayDee.
 Lady JayDee akitumbuiza katika show hiyo..
 Meneja wa Lady JayDee ambaye pia ni Mumewe Gadna Habash (kulia) akiwa na wasanii wa Bongo Movie.
 Jay Dee akikusanya fedha alizotunzwa na mashabiki wake na kumkabidhi mama yake.
 
 Lady Jay Dee akiwa katika pozi na mama yake mzazi.
Video ya show hiyo.
 Lady JayDee akiimba na Prof. J kibao chake cha Joto Hasira
 Judith Wambura akiimba na Mkongwe Hamza Kalala
 Prof J akikamua jukwaani sambamba na DJ Choka
 Hii ndo Anaconda Stile
 Mziki sio filamu kuwa mtu utakaa kitini na kuangalia bali mziki ni kucheza na hasa pale mashairi na midundo vinapo kukuna....Pichani ni Mashabiki wa burudani wakicheza show hiyo. Joyce Kiria na Salma Msangi Kimora wanayarudi vilivyo.

Hii ndio Team Anaconda ikiwa katika uzi wao makini
 Hivi ndivyo hali ilivyo ndani ya Ukumbi huu wa Nyumbani Lounge,Namanga jijini Dar es Salaam ambapo leo hii kuna bonge moja la show la Mwanadada mkongwe kwenye tasnia ya muziki hapa nchini,Lady Jay Dee ambaye anatimiza miaka 13 tangu alipoanza kazi yake ya muziki.katika show hii wanamuziki mbali mbali watapanda jukwaani aliwepo Mh. Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini,Mh. Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu.
 Wadau mbali mbali wa muziki hapa nchini wapo ndani ya ukumbi huu hivi sasa kusuhudia show hii ambayo ilikuwa ikisubiriwa kwa hamu na wapenzi wa muziki.
 Ndani ni nyomi la hatari,lakini nje nako watu bado wanataka kuingia huku wengi wao wakisema kuwa "hata kama hakuna siti,sie tuko radhi kusimama ilimradi tumsapoti Dada yetu.
 Getini mambo yako namna hii.
 Foleni bado ni ndefu na watu bado wanazidi kuingia ukumbini hapa hivi sasa.
Burudani ya Utangulizi ikiendelea.

No comments: