Monday, April 08, 2013

Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Katibu Mkuu wa CCM Abdurahamani Kinana Wampongeza Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula baada ya Kufunga Ndoa na Bi Yolanda

Waziri Mkuu Mizengo Pinda Akimpongeza Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara Philip Mangula na Mke wake Bi Yolanda MundA Mfupi baada ya kufunga ndoa, Kushoto juu ni katibu mkuu wa CCM COL:Mstaafu Abdurahaman Kinana
 Waziri Mkuu akimpongeza Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Philip Mangula baada ya kufunga ndoa na Bi Yolanda.
 Makamu Mwenyekiti Bara, Philip Mangula na Bi Yolanda wakati wa ibada ya ndoa yao.
 Maharusu wakiwa katika picha ya pamoja na wapambe wao.
--
Na Mwandshi Wetu
Waziri  Mkuu Mizengo Pinda amewataka wa Tanzania wapendane na kuishi kama watoto wa baba mmoja na kuondoa tofauti za kidini ambazo zina weza kulingiza taifa katika matatizo makubwa Waziri Mkuu ametoleamfano wahivi karibuni ambao badhi ya wakristo na waisilamu walianza kugombana kwa ajili ya uhalali wa kuchinja  amesema watanzania hawana budi kuheshimu imani za wenzao kwani miaka ya nyuma watu walikuwa wakishirikiana kiasi kwamba huwezi kujua tofauti ya mkristo na mwisilamu kwa vile watu walikuwa wana pendana nakuheshimu dini ya mwenzake , 

Hivyo amewaomba viongozi wadini kusaidia kurudisha upendo ambao  ulikuwepo amesema amefurahishwa na kuona hata viongozi wa dini ya kisilamu Kuwepo kanisani katika ibada ya kubariki ndoa ya Bwana Philip Mangula na Bibi Yolanda Kabelege amesema watu wanjombe ndio mfano wakuigwa

Waziri mkuu ameyasema hayo alipokuwa amehudhuria sherehe ya kubariki ndoa ya Makamu mwenyekiti wa ccm bara Mh Philip Mangula na Mwalimu Yolanda Kabelege ambayo imefanyika katika kanisa la Kilutheri Mkoani Njombe.

Naye Katibu mkuu wa ccm Mh Abdurahamani Kinana aliwapongeaza wana ndoahao kuamua jambo lakufunga ndoa kwani hata vitabu vitakatifu vinasema nyumba iliyo katika ndoa hata mungu huibariki nakuipa amani
 
Sherhe hiyo imefanyika siku ya jumamosi 6april 2013 ilhuduriwa na viongozi  dini wa chama na waserkali mabaozi na wana njombe 

No comments: