Friday, April 26, 2013

MBUNGE GODBLESS LEMA AKAMATWA NA POLISI





















Baada ya mabishano ya muda mrefu nyumbani kwa kada huyu na Mbunge wa Arusha mjini na uvamizi wa Polisi wakati huu wa usiku; Mh. Lema amekamatwa na amechukuliwa na gari la polisi na kupelekwa kituo kikuu cha polisi Arusha yaani Central Polisi.Wananchi wengi wamejitokeza ku-support mbunge wao.
Baada ya kumfikisha Lema Central police Arusha amesachiwa na kuingizwa ndani. Lema alikuwa ameambatana na magari ya wafuasi waliomsindikiza ili kushuhudia kinachojili hapo kituoni.Hivi sasa polisi wamewafukuza wafuasi wote hapo kituoni na kuwaambia hawatakiwi kuonekana hapo. 
wafuasi wameondoka kwa amani na kwenda kupaki Safari hoteli wakisubiriana kupata mwongozo.03:41amWamekutana pembeni ya kituo cha polisi na wamekubaliana kuwa watawanyike. Hivyo, Lema yupo ndani na wananchi waliomsindikiza wametawanyika kwenda kulala. Tutaonana asubuhi kwa yale yatakayojiri.

SOURCE.JAMII FORUM

No comments:

WAZIRI MKUU MHE. KASSIM MAJALIWA AMALIZA ZIARA YA SIKU MOJA MKOANI MBEYA

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb), leo ameondoka Mkoani Mbeya baada ya kukamilisha zi...