Friday, April 05, 2013

Mazishi ya Marehemu Nyaga Mawalla, yaliyofanyika jijini Nairobi Kenya katika Makaburi ya Jumuiya ya Langata

 Mwili wa marehemu Nyaga poul Mawalla ukiwa katika kanisa la Kilutheri nchini Kenya usharika wa Uhuru Highway kwa ajili ya misa
 Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe,Naibu Waziri wa Utalii na Maliasili Lazaro Nyarandu na Sir George kahama wakiwa kanisani wakishiriki misa ya maziko ya marehemu Nyaga Mawalla.
 Mbunge wa Jimbo la Arusha mjini Chadema  wa tatu kushot Mh Godbless Lema ni miongoni mwa waombolezaji waliokuwa kanisani nchini Kenya.
Mbunge wa Jimbo la Simanjiro wilani Simanjiro mkoani Manyara Christopher Ole Sendeka na Waziri wa zamani wa mambo ya ndani Laurence Marsha wakiwa kanisani nchini Kenya maziko ya marehemu Poul Mawalla 

 Kiongozi wa Dini wa Kanila la Kilutheri Kenya la Uhuru Highway akiongoza Mazishi.
  Jaji Mark bomani nae alikuwa ni miongoni mwa waombolezaji walioshiriki mazishi hayo.
  Sir George Kahama na mkewe wakiweka shada la maua katika Kaburi la Marehemu Nyaga Mawalla.
  Mwenyejiti wa Chadema, Freeman Mbowe na mkewe wakiweka shada la maua
 Wanafamilia wakiweka mashada ya maua
  Wabunge na Mawaziri mbalimbali wa serikali ya Jamhurti ya Muungano wa Tanzania, wakiweka mashada ya maua, pichani mbunge wa kahama -CCM James Lembeli akiweka shada la mau nyuma  yake ni naibu waziri wa maliasili na utaliii Lazaro Nyalandu
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu akiweka shada la Maua
  Balozi wa Tanzania nchini Kenya Dkt Batilda Burianiakiweka shada la maua
  Baadhi ya jamaa wa karibu wa Marehemu Nyaga ambao ni wabunge wakiweka Shada la Maua pichani ni mbunge wa Arusha Mjini -Chadema Mh Godbless Lema na Mbunge wa iringa Mjini Chadema Mchungaji Msigwa
 Familia ya Marehemu Nyaga Mawalla wakiwa wenye simanzi nzito wakati wa Mazishi hayo.
 Watoto wa Marehemu Nyaga wakiwa na ndugu zao.
Balozi wa Tanzania nchini Kenya Dkt Batilda Buriani akiwa na mwanasheria maarufu Jijini Arusha anayemiliki kampuni ya uwakili ya Law /Access Advocates Mosses Mahuna wakiwa nje ya kanisa la Lutherani nchini Kenya.
----
Mazishi ya Marehemu Nyaga Mawalla, aliyekuwa Mwasisi na Mkurugenzi wa Makampuni ya Mawalla ya Jijini Arusha yamefanyika jana jijini Nairobi Kenya katia Makaburi ya Jumuia ya Langata.

Mapema kabla ya Mazishi hayo yaliyohudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Serikali na familia na marafiki ilifanyika Misa ya kumuombea Marehemu katika Kanisa la KKKK, Uhuru Highway. 

Miongoni mwa Viongozi waliohudhuria Mazishi hayo ni Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Dk. Batilda Burian, Viongozi wastaafu, Sir. George Kahama, Mwemyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Wabunge, Mawaziri wanasheria mabalimbali wa ndani na nje ya Tanzania.

Marehemu Nyaga Paul Mawalla alifariki Machi 22, 2013 jijini Nairobi alikokuwaa amelazwa kwa matibabu  Hospitali ya Nairobi.

No comments: