Wednesday, April 17, 2013

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, Nape Nnauye Wafanya Kweli Ifakara mkoani Morogoro

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akifungua Shina la Wakereketwa  wa CCM la tawi la Manjechanga, Ifakara mkoani Morogoro, Aprili 17, 2013.

  Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akivishwa skafu na chipukizi alipowasili  eneo la kivuko cha Kilombero tayari kuanza ziara ya kikazi ya kuimarisha uhai wa chama hicho katika Wilaya ya Kilombero, mkoani Morogoro,Kinana alikuwa akitokea wilayani Ulanga.
 Katibu Mkuu wa NEC-CCM wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akiwa na watoto waliokuwa sehemu ya watu walioshuhudia  uzinduzi wa Tawi la CCM la Manjecha  eneo la Mahutanga, wilayani Kilombero.
 Katibu Mkuu wa NEC-CCM wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akipandisha bendera kuzindua rasmi Tawi la CCM la Manjecha  eneo la Mahutanga, wilayani Kilombero
 Aliyekuwa mwanachama wa Chadema, Julius Mogela akionyesha kadi yake, kwa wananchi kabla ya kumkabidhi Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (kushoto) baada ya kutangaza kuhamia CCM kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Aprili 17, 2013, kwenye stebdi ya mabasi, Ifakara mkoani Morogoro
Ranfred Majiji ambaye alikuwa mfuasi wa Chadema akikabidhiwa kadi ya CCM na Kinana
 Anna Mwakitosi aliyekuwa mwanachama wa Chadema, Anna Mwakitosi akishangiliwa na wafuasi wa CCM baada ya kujiunga CCM
 Kinana akihutubia katika mkutano wa hadhara uliofanyika Stendi ya Ifarakara Mjini

Sehemu ya umati wa wananchi uliofika kwenye mkutano huo
 Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Elias Masala (kulia), akijibu maswali mbele ya Kinana jinsi alivyopanga mikakati ya kuwaletea mandeleo wananchi wa wilaya hiyo.
.Baadhi ya wafuasi wa Chadema wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM, alipohutubia mkutano mkubwa wa hadhara kwenye Stendi ya mabasi ya Ifakara mkoani Morogoro, Aprili 17, 2013.
Baadhi ya wafanyabiashara walilazimika kusitisha shughuli zao kumsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana alipohutubia mkutano mkubwa wa hadhara kwenye stenbdi ya mabasi, Ifakara mkoani Morogoro. Pichani ni wauza ndizi wakiwa kwenye mkutano huo, Aprili 17, 2013.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akipiga ngoma wakati wa uzinduzi wa Shina la Wakereketwa  wa CCM la tawi la Manjechanga, Ifakara mkoani Morogoro, Aprili 17, 2013.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (kulia), akimkabidhi ubani mtoto wa aliwahi kuwa Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kilombero, marehemu Oswald Mkokochela, Edward wakati uongozi wa chama hicho ulipokwenda jana  kuifariji familia kwa msiba wa uliotokea juzi. Ifakara Mjini,
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Morogoro, Innocenti Kalogaries akimkabidhi ubani Edward.Picha na Richard Mwaikenda na Bashir Nkromo

No comments: