Wednesday, July 14, 2010

Soko la Pamoja EAC bado


NAIBU Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Beatrice Kiraso akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa idara ya habari maelezo ambapo amesema soko la pamoja la jumuiya hiyo bado halijaanza rasmi kama inavyodhaniwa kwasababu kuna mambo mengi ambayo hayajakamilika.

Kiraso ambaye anashughulikia shirikisho la kisiasa la jumuiya hiyo alisema jijini Dar es Salaam jana kuwa, soko hilo liliidhinishwa kuanza Julai Mosi mwaka huu lakini bado kuna mambo mengi ambayo hayajakamilika. (Picha na Mwanakombo Jumaa)-MAELEZO.

1 comment:

Anonymous said...

I would like to exchange links with your site charaz.blogspot.com
Is this possible?