Wednesday, July 14, 2010

Breaking News Profesa Mwaikusa auawa na majambazi


Taarifa zilizotufikia muda mfupi uliopita zinaeleza kuwa yule nguli na mwanasheria ambaye pia ni Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu aliyetikisa katika kesi ya mgombea binafsi, Profesa Jwani Mwaikusa ameuawa kwa kupigwa risasi na majambazi waliovamia nyumbani kwake majira ya saa nne usiku.

Sambamba na mauaji ya Profesa huyo majambazi hayo pia yaliua mtoto aliyekuwamo ndani ya nyumba ya Profesa huyo na kisha kumuua jirani kwa kumpiga risasi, haijafahamika yamepora mali gani na nini lengolao hasa, mamlaka za serikali bado hazijathibitisha tukio hilli, taarifa hii imepatikana kutoka kwa ndugu wa karibu wa Profesa huyo.

3 comments:

makengeza said...

Mungu wangu, siamini ... sitaki kuamini ... Jwani jamani. Kwa nini? Kwa nini?

Naomi said...

Jwani ameniuma sana kwa kifo chake, pia Gwamaka mpwa wake.. Mungu alipize kisasi na Haki itendeke.. Rest In Peace Jwani and Gwamaka na Jirani pia.

Unknown said...

Ninachokiamini hao jamaa hawana muda mrefu watakamatwa tu, maana damu ya mwanadamu aliyeumbwaa na Mungu haimwagiki hivihivi tu, siku mija watajitaja tu,,hata miezi miwili haiishi..
Thomas Temi