Thursday, April 29, 2010

Ajali mbaya::WANAFUNZI 18 WAFA, 125 WAJERUHIWA


Wahudumu wa hospitali ya Bombo wakimpeleka majeruhi katika chumba cha upasuaji baada ya kujeruhiwa katika ajali ya gari aina ya Fuso lililokuwa likiwasafirisha wanafunzi wa chuo cha kiislamu cha Shamsil-Maariff cha Duga Jijini Tanga waliokuwa wakitokea kwenye Maulid yaliyofanyika Kijiji cha Kibafuta kilichopo mpakani mwa Wilaya ya Tanga na Mkinga jumla ya umla ya wanafunzi 18 walikufa na wengine 125 walijeruhiwa.

Mmoja wa majeruhi akiwa chini ya uangalizi wa daktari mtaalamu kutoka nje ya nchi majeruhi huyo ambaye jina lake halikuweza kupatikana alipata ajali baada gari aina ya Fuso lililokuwa likiwasafirisha wanafunzi wa chuo cha kiislamu cha Shamsil-Maariff cha Duga Jijini Tanga waliokuakiwa katika wodi ya Galanosi Hospitali ya Bombo baada ya gari aina ya Fuso lililokuwa likiwasafirisha wanafunzi wa chuo cha kiislamu cha Shamsil-Maariff cha Duga Jijini Tanga waliokuwa wakitokea kwenye Maulid yaliyofanyika Kijiji cha Kibafuta kilichopo mpakani mwa Wilaya ya Tanga na Mkinga jumla ya umla ya wanafunzi 18 walikufa na wengine 125 walijeruhiwa.

Majeruhi Ali Maulid akiwa katika wodi ya Galanosi Hospitali ya Bombo baada ya gari aina ya Fuso lililokuwa likiwasafirisha wanafunzi wa chuo cha kiislamu cha Shamsil-Maariff cha Duga Jijini Tanga waliokuwa wakitokea kwenye Maulid yaliyofanyika Kijiji cha Kibafuta kilichopo mpakani mwa Wilaya ya Tanga na Mkinga jumla ya umla ya wanafunzi 18 walikufa na wengine 125 walijeruhiwa. Imeandikwa na Burhan Yakubu.

*********************************************************

JIJI la Tanga limfeunikwa na simamzi kuu kufatia wanafunzi 18 wa Chuo cha Kiislamu cha Shamsil-Maariff kufa papo hapo na wengine 125 kujeruhiwa vibaya, baada ya lori walilokuwa wakisafiria kutoka kwenye sherehe za maulidi kupinduka.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Adolphina Kapufi aliliambia gazeti hli jana kuwa ajali hiyo ilitokea saa 5:30 usiku wa kuamkia jana katika eneo la njiapanda kuu ya Mabanda ya Papa jijini hapa.

Kapufi aliwataja baadhi ya waliokufa katika ajali hiyo kuwa ni Twalib Kunemu, Juma Idd, Faraji Habib, Jahshi Rashid, Hussein Bakari, Hajji Athumani naYussuph Hussein na kwamba, kazi ya kuwatambua maiti wengine bado inaendelea.

Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Paschal Kanyinyi alisema kazi ya kuwatambua waliokufa na majeruhi waliolazwa katika hospitali hiyo wodi ya Galanosi inaendelea.

Kanyinyi aliwataja majeruhi waliotambuliwa kuwa ni Jumaa Salim ambaye ameumia mbavu, Makame Ahmed, Ahmed Shehe, Selemani Said na Juma Akida.

Aliwataja majeruhi ambao hali zao ni mbaya, hivyo waliokimbizwa katika Hospitali Taifa ya Muhimbili, jijini Dar essalaam kuwa ni Hemed Shaaban na Hassan Adam.

Kanyinyi alifahamisha kuwa kati majeruhi 125 walifikishwa katika hospitali hiyo usiku wa kuamkia jana baada ya kupata ajali, 70 walipata matibabu na kuruhusiwa kurejea chuoni kwao.

Kwa mujibu wa Kaimu Mganga Mkuu huyo, majeruhi 55 wanaendelea kupata matibabu katika hospitali hiyo kwa msaada wa timu maalumu ya waganga na wauguzi waliokusanywa kutoka hospitali na vituo mbalimbali vya afya mkoani Tanga kwa ajili ya kutoa huduma hiyo.

Mwananchi ilifika katika Hospitali hiyo ya Bombo na kukuta idadi kubwa ya wananchi waliokusanyika katika hospitali hiyo kwa lengo la kutambua miili ya waliokufa na majeruhi.

Mwalimu wa zamu wa Chuo hicho, Ustaadh Ajali Ramadhan, alisema kuwa wanafunzi hao walikuwa wakitokea Kijiji cha Kibafuta ambako walikwenda kuhudhuria sherehe za kuzaliwa kwa Mtume Mohamad S.A.W.

No comments: