Tuesday, April 06, 2010

Rais Kikwete apindua maamuzi ya UWT

RAIS Jakaya Kikwete amepindua maamuzi ya UWT walimbwaga Husna Mwilima, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanawake (UWT), kwa kashfa na kejeli wakidai hafai, sasa Mwilima ameula na anakuwa DC mpya wa Tandahimba wakati huo huo amefanya mabadiliko ya vituo vya kazi kwa baadhi ya Wakuu wa Wilaya nchini kwa kuwahamisha na kuwapangia vituo vipya kama ifuatavyo:-

1. Gishuli M. Mbegesi - Njombe amepangiwa kwenda Kilindi
2. Leonidas T. Gama - Mbeya amepangiwa kwenda Ilala
3. Frank A. Uhaula - Tarime ameoangiwa kwenda Kiteto
4. Bi. Sarah Dumba - Kilindi amepangiwa kwenda Njombe
5. John B. Henjewele - Kiteto amepangiwa kwenda Tarime
6. Rashid M. Ndaile - Chunya amepangiwa kwenda Mkinga
7. Evans Balama - Ilala amepangiwa kwenda Mbeya
8.Florence A. Horombe -Bukombe amepangiwa kwenda Nzega
9. Bi. Zainab Kwikwega -Kasulu amepangiwa kwenda Makete
10. Bi. Hawa Ngh’umbi -Makete amepangiwa kwenda Bukombe
11. Lt. Col. John Mzurikwao -Mpanda amepangiwa kwenda Sumbawanga
12. Bi Betty Machangu -Nzega amepangiwa kwenda Kasulu
13. Dk. Rajab Lutengwe -Ulanga amepangiwa kwenda Mpanda
14. Francis Miti -Tandahimba amepangiwa kwenda Ulanga
15. Deodatus Kinawiro -Mkinga amepangiwa kwenda Chunya

Taarifa ya uteuzi huo iliyosainiwa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Bw. Aggrey Mwanri imesema pamoja na mabadiliko hayo, Rais Kikwete pia amemteua Bibi Husna Mwilima aliekuwa Katibu mkuu wa Umoja wa Wanawake kuwa Mkuu wa Wilaya ya Tandahimba kuchukua nafasi ya Ndugu Francis Miti ambaye anahamia wilaya ya Ulanga.

Aidha, Rais Kikwete ametengua uteuzi wa Bw. Thobias M. Sijabaje ambaye alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga kutokana na kutosimamia vizuri zoezi la ugawaji wa vocha za pembejeo za kilimo katika wilaya ya Sumbawanga katika msimu wa mwaka 2009/2010.

Mabadiliko haya yanakusudia kuongeza ufanisi wa kazi, kuimarisha utendaji katika wilaya hizo na yanaanza mara moja.


Imetolewa na:
Ofisi ya Waziri Mkuu,
S. L. P. 3021
DAR ES SALAAM
Jumanne, Aprili 06, 2010.

No comments: