Sunday, October 18, 2009

Kunduchi Beach Hotel & Resort Kudhamini Miss East Africa 2009!!



Cefora kulia na Selemawit washiriki kutoka Eritrea.
Kunduchi Beach Hotel & Resort itadhamini mashindano ya kimataifa ya Miss East Africa 2009 yatakayo fanyika mwezi Desemba mwaka huu jijini Dare s salaam, Tanzania.
Kwa udhamini huo, Kunduchi Beach Hotel & Resort ndiyo inakuwa OFFICIAL RESIDENCE ya Miss East Africa 2009 ambapo
warembo wote kutoka Nchi 14 zinazoshiriki mashindano hayo watafikia na kuishi katika hoteli hiyo ya kifahali iliyo kandokando ya ufukwe wa bahari ya hindi.
“Tunapenda kushukuru uongozi wa Kunduchi Beach Hotel & Resort kwa kudhamini mashindano yetu ya mwaka huu ampapo sasa wasichana wetu tatafikia katika hiyo ambayo ni moja ya hoteli za kuvutia barani Afrika”
Mashindano ya MISS EAST AFRICA 2009 yamepangwa kufanyika tarehe 18 mwezi Desemba mwaka huu katika ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es salaam.
Mashindano hayo yatashirikisha warembo 28 kutoka Nchi 14 zilizo katika ukanda wa Afrika mashariki ambazo ni pamoja na wenyeji TANZANIA, KENYA, UGANDA, RWANDA na BURUNDI. Zingine ni ETHIOPIA, ERITREA, DJIBOUTI, SOMALIA, pamoja na visiwa vya MAURITIUS, MADAGASCAR, COMOROS, RE UNION na SEYCHELLES.
Taji la Miss East Africa kwa sasa linashikiliwa na mrembo Claudia Niyonzima wa Burundi aliyeshinda mashindano hayo mwaka jana jijini Bujumbura.
Tunapenda pia kuwakumbusha watu wote kwamba ile bahati nasibu ya MISS EAST AFRICA ya kusaidia yatima bado inaendelea na unaweza kujishindia zawadi mbalimbali kwa kununua tiketi za bahati nasibu hiyo kupitia kwa wauzaji wa magazeti kote Nchini au kwa kutuma neno “SHINDA” kwa sms kwenda namba 15567 kupitia simu za mkononi.
Zawadi ya juu kabisa katika bahati nasibu hiyo ni gari aina ya Range Rover Sport kutoka kampuni ya CMC Automobile Ltd.
“Tunapenda kuwahakikishia wapenzi wa fani ya urembo kwamba mashindano ya MISS EAST AFRICA mwaka huu yatakuwa ya kuvutia sana na yenye ushindani mkubwa kwa vile kila Nchi imekusudia kuleta warembo bora na wenye viwango vya juu katika fani hiyo”
Kwa ujumla maandalizi kwa ajili ya mashindano hayo yanakwenda vizuri;
Aidha, kampuni ya AKO Catering services ndiyo itakayo toa huduma ya chakula na vinywaji ndani ya ukumbi wa Mlimani City siku ya fainali ya mashindano ya Miss East Africa 2009.
“Tumeamua kuitumia kampuni ya AKO catering services kwa huduma hiyo ili kuhakikisha kwamba watu wote siku hiyo wanapata huduma bora kabisa ukumbini hapo. AKO ndiyo kampuni bora hapa Nchini kwa shughuri za chakula na vinywaji”
Fainali za mashindano ya MISS EAST AFRICA 2009 zinasubiliwa kwa hamu na wapenzi wa fani hiyo barani Afrika na inatarajiwa kwamba watu wapatao millioni 200 wataangalia mashindano hayo kupitia katika Television barani Afrika.
Kituo cha East Africa Television ndiyo official TV station ya mashindano ya MISS EAST AFRICA.

No comments: