Monday, October 02, 2017

VODACOM TANZANIA YASHEREHEKEA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA NA WATEJA WAKE

 Mkuu wa kitengo cha maduka ya rejareja ya Vodacom Tanzania PLC, Brigita Stephen akikata utepe kuashiria uzinduzi wa dawati la huduma kwa wateja wa kampuni hiyo”Service desk”lililopo soko la makumbusho jijini Dar es Salaam katika kusherehekea wiki ya huduma kwa wateja inayoanza kufanyika leo dunia nzima,Wanaoshuhudia kutoka kushoto Meneja wa kampuni hiyo,Fredrick Laini,Mteja na mkazi wa Makumbusho,Alex Kisanga.
 Alex Kisanga(kulia)Ambaye ni Mteja wa kwanza kufika katika dawati la huduma kwa wateja wa Vodacom Tanzania PLC,”Service desk”lililopo soko la makumbusho jijini Dar es Salaam,Akionyeshwa baadhi ya bidhaa zilizopo katika dawati hilo baada ya kuzinduliwa rasmi na Mkuu wa kitengo cha maduka ya rejareja ya kampuni hiyo, Brigita Stephen(katikati)na Meneja wa kampuni hiyo,Fredrick Laini,katika kuazimisha wiki ya huduma kwa wateja inayoanza leo na  kufanyika dunia nzima.
 Mteja wa Vodacom Tanzania PLC,Dkt. Mdimu Ngoma akishirikiana na Mkuu wa kitengo cha maduka ya rejareja wa kampuni hiyo, Brigita Stephen,kukata keki ikiwa ni ishara ya kusherehekea wiki ya huduma kwa wateja inayoanza leo na kufanyika dunia nzima.
 Mkuu wa kitengo cha maduka ya rejareja wa Vodacom Tanzania PLC,Brigita Stephan(katikati)akimlisha keki mteja wa kampuni hiyo Dkt. Mdimu Ngoma ikiwa ni ishara ya kusherehekea wiki ya huduma kwa wateja duniani inayoanza leo. 
 Baadhi ya wafanyakazi wa Vodacom Tanzania PLC,Wakiwa kwenye picha ya pamoja wakati wakusherehekea wiki ya huduma kwa wateja inayoanza leo na kufanyika dunia nzima.
Meneja wa duka la Vodacom Tanzania,tawi la Mlimani city jijini Dar es salaam,Vanessa Mlawi akipiga selfie na wafanyakazi wenzake na wateja wa kampuni hiyo katika kusherehekea wiki ya huduma kwa wateja inayoanza leo na  kufanyika dunia nzima.

No comments: