Thursday, October 19, 2017

KANGI LUGOLA AKUTANA NA MAKAMU WA RAIS

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mhe. Kangi Lugola (kushoto) na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Faustine Kamuzora  (kulia) mara baada ya mazungumzo ambapo  Mhe. Kangi Lugola alijitambulisha  kwa mara ya kwanza kama Naibu wa Wizara hiyo kwa Makamu wa Rais. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais). 
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Mhe. Kangi Lugola (katikati)akitembea kwa miguu akielekea ofisini kwake barabara ya Luthuli mara baada ya kumaliza mazungumzo na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Faustine Kamuzora. (picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)

No comments:

RAIS SAMIA ASHIRIKI NA KUTUNUKU TUZO ZA WASANII WA KOMEDI TANZANIA 2025

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameshiriki kama mgeni rasmi katika hafla ya utoaji wa Tuzo za Wasa...