Monday, October 02, 2017

UTAFITI WA KILIMO KUFANYIKA NCHI NZIMA KUANZIA KESHO

 Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS)  Dkt. Albina Chuwa akizungumza wakati wa kufunga mafunzo ya wadadisi wa Utafiti wa Takwimu za Kilimo kwa mwaka 2016/17 mkoani Dodoma. Utafiti huo wa Takwimu za Kilimo utafanyika nchi nzima kuanzia  tarehe 3 Oktoba na kumalizika tarehe 3 Novemba, 2017. 
 Mgeni rasmi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Dkt. Maria Mashingo akihutubia wakati wa kufunga mafunzo ya wadadisi wa Utafiti wa Takwimu za Kilimo kwa mwaka 2016/17 mkoani Dodoma. Utafiti huo wa Takwimu za Kilimo utafanyika nchi nzima kuanzia  tarehe 3 Oktoba na kumalizika tarehe 3 Novemba, 2017. 
 Baadhi ya wadadisi wa Utafiti wa Takwimu za Kilimo kwa mwaka 2016/17 wakifuatilia kwa makini hotuba ya mgeni rasmi (hayupo pichani) wakati wa kufunga mafunzo ya utafiti huo mkoani Dodoma. Utafiti huo wa Takwimu za Kilimo utafanyika nchi nzima kuanzia  tarehe 3 Oktoba na kumalizika tarehe 3 Novemba, 2017. 
 Mgeni rasmi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Dkt. Maria Mashingo (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa NBS, Chuo cha Mipango na baadhi ya wadadisi wa Utafiti wa Takwimu za Kilimo kwa mwaka 2016/17.  Utafiti huo wa Takwimu za Kilimo utafanyika nchi nzima kuanzia  tarehe 3 Oktoba na kumalizika tarehe 3 Novemba, 2017. 
Mwanasheria wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS)  Oscar Mangula akiwaapisha wadadisi wa Utafiti wa Takwimu za Kilimo kwa mwaka 2016/17 baada ya kufunga mafunzo ya utafiti huo mkoani Dodoma. Utafiti huo wa Takwimu za Kilimo utafanyika nchi nzima kuanzia  tarehe 3 Oktoba na kumalizika tarehe 3 Novemba, 2017.

Na: Veronica Kazimoto
Serikali kupitia Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) inatarajia kufanya Utafiti wa Kilimo wa mwaka 2016/17 nchi nzima kuanzia kesho tarehe 3 Oktoba hadi tarehe 3 Novemba, 2017. 

Akizungumza leo wakati wa kufunga mafunzo ya wadadisi watakaokusanya Takwimu za Kilimo kwa mwaka 2016/17 mkoani Dodoma, Katibu Mkuu, Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Dkt. Maria Mashingo amesema lengo la utafiti huo ni kutoa makadirio ya kiasi cha uzalishaji wa mazao makuu, idadi ya mifugo, mazao yatokanayo na mifugo na maeneo ya kilimo katika mikoa yote ya Tanzania.

"Ningependa kuwasisitizia washiriki kuwa, dhumuni kubwa la utafiti huu wa  kilimo ni kutoa makadirio ya uzalishaji wa mazao makuu ya kilimo na maeneo yake yaliyolimwa pamoja na taarifa za mifugo katika mikoa yote ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania", amesema Dkt. Mashingo.

Aidha, Katibu Mkuu huyo ametoa wito kwa wakuu wote wa kaya watakaochaguliwa kushiriki kwenye utafiti huu, kutoa ushirikiano wa kutosha na hususan kutoa taarifa sahihi kuhusu hali ya uzalishaji wa mazao, huduma zinazotolewa na Maafisa Ugani na aina ya mbegu wanazotumia na kubainisha changamoto wanazokumbana nazo katika shughuli zao za kila siku.

Nae Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa amesema jumla ya wadadisi 600 wamepatiwa mafunzo ya siku 5 kwa ajili ya kufanya utafiti huo nchi nzima.

Dkt. Chuwa amefafanua kuwa madhumuni ya mafunzo kwa wadadisi hao ni kuwajengea uwezo wa kuhoji na kujaza madodoso ya wamiliki wa mashamba (wakulima) na namna ya kutambua mahali shamba lilipo kwa kutumia kifaa maalumu kiitwacho GPS.



Utafiti huu wa Kilimo wa mwaka 2016/17 unafanyika chini ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu, Zanzibar (OCGS) kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji. 

No comments: