Tuesday, October 31, 2017

MATUKIO KATIKA PICHA ZA KIKAO CHA KAMATI YA UTAWALA NA SERIKALI ZA MITAA MJINI DODOMA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala, Mheshimiwa George Mkuchika akisoma Taarifa ya Maboresho ya Mfumo wa Utumishi na Mshahara Serikalini (MCMIS) wakati Kamati hiyo ilipokutana na Kamati ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Mjini Dodoma. Kulia kwake ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Laurean Ndumbaro.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa akifuatilia majadiliano ya Wajumbe wa Kamati yake wakati Kamati hiyo ilipokutana na Waziri wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala kwa ajili ya kupokea na kujadili Taarifa ya Maboresho ya Mfumo wa Utumishi na Mshahara Serikalini (MCMIS), Kulia kwake ni Katibu wa Kamati hiyo, Eunike Shirima.
Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa wakiwa katika kikao na Watendaji wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala ambapo leo walijadili Taarifa ya Maboresho ya Mfumo wa Utumishi na Mshahara Serikalini (MCMIS), Kulia kwake ni Katibu wa Kamati hiyo, Eunike Shirima.

No comments:

MAJALIWA MGENI RASMI MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA TEWW

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Oktoba 25, 2025 ni mgeni rasmi katika kongamano la kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya Taasisi ya Elimu y...