Friday, May 12, 2017

RAIS WA AFRIKA KUSINI JACOB ZUMA AWASILI IKULU JIJINI DAR ES SALAAM NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MWENYEJI WAKE RAIS DKT. MAGUFULI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mgeni wake Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma wakati wa Nyimbo za Mataifa mawili (Tanzania & Afrika Kusini)  zikipigwa katika viwanja wa Ikulu jijini Dar es Salaam. 
 Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma akipita kukagua Gwaride la Heshima aliloandaliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na mgeni wake Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma wakati wakiangalia vikundi vya ngoma za asili vilivyokuwa vikitumbuiza ndani ya viwanja vya Ikulu kwa Heshima ya ugeni huo wa Rais wa Afrika Kusini.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na mgeni wake Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma kabla ya kuanza mazungumzo yao Rasmi Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na mgeni wake Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma wakati wakielekea kwenye ukumbi wa mkutano kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali ya Kimaendeleo yahusuyo mataifa hayo mawili ya Tanzania na Afrika Kusini.
 Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma akipunga mkono wakati akiwasili Ikulu akiwa pamoja na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wanahabari mara baada ya kumaliza mazungumzo na mgeni wake Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma, Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma kabla ya kuanza kuzungumza na wanahabari Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma akisoma hotuba yake wakati akizungumza na wanahabari Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru mgeni wake Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma mara baada ya kuzungumza na wanahabari Ikulu jijini Dar es Salaam.
  Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma akipiga ngoma wakati alipowasili Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma akizungumza jambo na Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Rais Dkt. John Pombe Magufuli
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Mama Sizakele Zuma Mke wa Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma mara baada ya kufika ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akifurahia jambo pamoja na Mama Sizakele Zuma Mke wa Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma aliyeambatana na msaidizi wake Ikulu jijini Dar es Salaam.
Vikundi vya Matarumbeta vikitoa burudani wakati Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma alipowasili Ikulu jijini Dar es salaam. PICHA NA IKULU

No comments: