Saturday, December 10, 2016

Ridhiwani Kikwete aendelea na Ziara Jimboni kwake Chalinze

Mbunge wa Jimbo la Chalinze Mh Ridhiwani Kikwete ameendelea na ziara yake ya kushtukiza katika Jimbo lake kukaguwa miradi ya kimaendeo, Desemba 9 amezunguka katika Zahanati na Shule za Secondary Chalize pamoja na mradi wa ufugaji kuku katika Kata ya Msoga ili kuona utendaji kazi pamoja na miradi ambayo inafanyika pia kuzichukua changamoto zilizopo na kuangalia jinsi ya kuzitatua.
Mh Mbunge Ridhiwani alitembelea katika Hospital ya Msoga ambayo ilijengwa na Rais Mstaafu Dr. Jakaya Mrisho Kikwete. Kupitia Ofisi ya Mbunge walitoa vifaa tiba katika Hospital hiyo ikiwamo X-RAY machine, Ado sound Mashine, Vitanda 70,Bed cover, Vitanda zaidi ya 70, mashine za dawa za usingizi zaidi ya tano, mafriji ya kuifadhia damu matatu, kiti kwa ajili ya tiba ya meno na vifaa vingine vingi.

Hospital ya Msoga inatarajiwa kuwa ya wilaya baada ya kukamilisha baadhi ya vitu ikiwemo samani, inaupungufu wa mabenchi ya kukalia wagonjwa 150, viti 150, Meza 40, na Mashelfu ya kuifadhia dawa pamoja na AC katika chumba hicho kwa ajili ya kuifadhia dawa, Ukosefu wa kichomea taka hatarishi pamoja na Mochwari Lakini pia kuna changamoto ya umaliziaji wa chumba cha kuifadhia digital x-ray machine ambayo ni kubwa iliyotolewa na Mh Mbunge
Baadhi ya Dawa kaaika Chumba cha kuifadhia Dawa Hospital ya Msoga
 
Kiti cha matibabu ya meno mbacho kilitilewa na Ofisi ya Mbunge katika Hospital ya Msoga
Mh Mbunge akitoa maelekezo kwa team aliyoongozananayo katika ziara yake ya kushtukiza kukaguwa miradi ya kimaendeo
Mh Mbunge pamoja team yake na madaktari wa hospital ya Msoga wakiangalia shimo la utupaji taka hatarishi katika hospital hiyo alipofanya ziara ya kushtukiza kukaguwa miradi ya kimaendeleo katika Jimbo lake.
Mh Mbunge na madaktari na wafanya kazi wa hospital ya Msoga katika picha ya pamoja badaa ya kukaguwa mirada ya kimaendeleo na utekelezaji wa miradi hiyo katika hospital ya Msoga.
Mh Mbunge akisaini kitabu cha wageni baada ya kuingia katika Shule ya secondary Lugoba akiwa katika ziara ya kushtukiza kukaguwa miradi ya kimaendeo
Mh Mbunge akizungumza jambo na mwalimu mkuu wa Shule ya secondary Lugoba Abdalla Sakasa
 
Mh Mbunge akitoa maelekezo kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondary Lugoba Abdallah Sakasa, pamoja na Team yake aliyoongozana nayo alipokuwa akikaguwa nyumba za walimu ambazo zilijengwa chini ya Ofisi ya Mbunge katika ziara yake ya kushtukiza kukaguwa miradi ya kimaendeo
Matank ya Maji kwa matumizi ya Shule pamoja na walimu katika Shule ya Secondary Lugoba.
 
Chumba cha Darasa la Kompyuta katika Shule ya Sekondary Lugoba
 
Mh Mbunge Ridhiwani akiangalia Kiti cha matibabu ya Meno katika Dispensary ya shell ya Secondary Lugoba.
Mh Mbunge akiwa katika eneo ambalo litajengwa tank kubwa la maji litakalo sambaza maji mji mzima wa chalize kutokea Ruvu.
Uchimbaji na Uwekaji maboba ya maji kutokea Ruvu kuja Chalinze ukiendelea.
 
Mh Mbunge akisalimiana na moja ya ijinia alipotembelea eneo la ujenzi wa Kiwanda cha uchakataji matunda
Mh Mbunge akiwa anapewa maelekezo baada kutembelea eneo la ujenzi wa Kiwanda cha uchakataji matunda
   
Nyumba za walimu zikiwa zimemalizika katika Shule ya Secondary Merento
Vyumba vya Madarasa vilivyojengwa chini ya ofisi ya mbunge katika shule ya secondary Morento.
Nyumba za walimu zilivyojengwa chini ya ofisi ya mbunge katikakatika Shule ya Secondary Morento.
Nyumba za walimu zilizopo katika hatua za mwisho za ujenzi katika Shule ya Secondary Morento.
Mh Mbunge akitoa maelekezo kea team yake katika Nyumba za walimu zilizopo kwenye hatua za mwisho za ujenzi katika shule ya Secondary Morento.
Bweni la wasicha lilounguwa kwa moto katika shule ya secondary Morento
Mh Mbunge akipokea taarifa ya mradi wa ufugaji kuku katika Kata ya Msoga
Mh Mbunge akipokea kuku wa kitoweo baada ya kumaliza kukaguwa mradi kuku katika Kata ya Msoga

No comments: