Sunday, December 04, 2016

TRA YASHINDA TUZO YA UTUNZAJI BORA WA MAHESABU KWA TAASISI ZA UMMA

 Naibu Mkurugenzi wa Idara ya Fedha (TRA) Bi. Anna Mndeme kulia akipokea tuzo ya utunzaji bora wa mahesabu kwa taasisi za umma  kutoka kwa Mwakilishi wa Mhasibu Mkuu wa Serikali  Bw .Shogolo Msangi katikati  wakati wa sherehe za kukabidhi tuzo hizo kwa  wawasilishaji bora wa mapato kwa mwaka 2015 yaliyofanyika nje kidogo ya jiji la Dar es salaam wa kwana kushoto ni Mwenyekiti wa NBAA Prof. Isaya Jairo.
 Mkurugenzi wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) Dkt.Ayoub Rioba kulia akipokea tuzo ya utunzaji bora wa mahesabu kwa taasisi za umma baada kuwa mshindi wa pili  kutoka kwa kwa Mwakilishi wa Mhasibu Mkuu wa Serikali  Bw .Shogolo Msangi kushoto  wakati wa sherehe za kukabidhi tuzo hizo kwa  wawasilishaji bora wa mapato kwa mwaka 2015 yaliyofanyika nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.
 Afisa Mkuu wa Mapato kutoka kampuni ya kutengeneza sementi (Tanga Cement Plc) Bw. Pieter De Jager wa pili kulia akiwa ameshika tuzo ya washindi wa jumla kwenye masindano ya wawasilishaji bora wa mapato kwa mwaka 2015 yaliyofanyika nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.

 Mwakilishi wa Mhasibu Mkuu wa Serikali  Bw .Shogolo Msangi katikati waliokaa  akiwa katika picha ya pamoja na washindi wa uwasilishaji bora wa mapato  wakati wa sherehe za kukabidhi tuzo hizo kwa mwaka 2015 iliyofanyika nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.Picha Na Ally Daud-Maelezo

Na Ally Daud-MAELEZO
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imeshinda tuzo ya utunzaji bora wa mahesabu kwa taasisi za umma  zilizoandaliwa na   Bodi ya Ukaguzi na Wahasibu (NBAA) kwa mwaka 2015. 

Akipokea tuzo hiyo Naibu Mkurugenzi wa Idara ya Fedha (TRA) Bi. Anna Mndeme amesema kuwa wamepata tuzo hiyo kutokana na  kuwasilisha vizuri mahesabu ya mwaka wa fedha yaliyowasilishwa kufuatana na viwango vya uwasilishwaji  vinavyozingatiwa na Bodi ya Ukaguzi na Wahasibu (NBAA).

“Tumefanya vizuri na tumepata tuzo kwa kushika nafasi ya kwanza kutokana na  kuwasilisha vizuri mahesabu ya mwaka wa fedha yaliyowasilishwa kufuatana na viwango vya uwasilishwaji  vinavyozingatiwa na Bodi ya Ukaguzi na Wahasibu (NBAA)” alisema Bi. Mndeme.

Aidha Bi. Mndeme amesema kuwa tuzo hiyo ni chachu kwa TRA itayofanya waendelee kujituma zaidi katika ukusanyaji na utunzaji wa mapato ili kusaidia nchi kupata huduma bora za jamii kwa maendeleo ya taifa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi TRA Bw. Richard Kayombo amesema kuwa huo ni uthibitisho kwamba TRA inafanya kazi  kwa ueledi na uwazi kupelekea kupata tuzo ya heshima.
Katika mashindano hayo Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) wameibuka washindi wa pili huku kampuni inayotengeneza Sementi  (Tanga Cement Plc) wakiibuka kuwa washindi wa jumla kwenye tuzo hizo .

No comments: