Thursday, December 08, 2016

Magari 4 Yagongana Mbeya, ni Basi la Abiria, Malori Mawili ya Mizigo na Pick-Up

ajali1
ajali2
ajali3
ajali4
MBEYA: Basi la abiria mali ya Kampuni ya New Force, malori mawili ya mizigo (ambapo moja ni aina ya Scania lenye namba za usajili T 103 ATX) na gari dogo aina ya Toyota Pick-up yamegongana na kusababisha ajali leo asubuhi katika eneo la Igurusi mkoani Mbeya.
Taarifa zimeeleza kuwa, basi hilo la New Force lilikuwa likitokea Tunduma kuelekea jijini Dar es Salaam likiwa na abiria wake na hakuna mtu yeyote aliyeripotiwa kupoteza maisha kutokana na ajali hiyo.

No comments:

BILIONEA ROSTAM AZIZI AANDIKA HISTORIA: ACHUKUA UMILIKI MKUBWA WA NATION MEDIA GROUP, AFUNGUA ENZI MPYA YA UWEKEZAJI WA KIMKAKATI AFRIKA MASHARIKI

Mfanyabiashara maarufu nchini TANZANIA , Rostam Aziz , ameandika historia mpya katika sekta ya habari baada ya kukamilisha ununuzi wa hisa a...