Thursday, December 08, 2016

BALOZI WA CUBA AMUAGA WAZIRI MWAKYEMBE

 Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akimpatia kadi ya mawasiliano Mgeni wake Balozi wa Cuba Mhe. Jorge Luis Lopez alipofika ofisini kwake leo (8/12/2016) kwa ajili ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kazi hapa nchini.
 Balozi wa Cuba Mhe. Jorge Luis Lopez akiandika ujumbe wa kumuaga Waziri  wa Mambo ya Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe kwenye kitabu cha wageni ofisini kwa Waziri huyo alipofika kwa ajili ya kumuaga.
Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akibadilishana mawazo na Mgeni wake Balozi wa Cuba Mhe. Jorge Luis Lopez  alipofika ofisini kwake leo (8/12/2016) kwa ajili ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kazi hapa nchini.

No comments: