Tuesday, August 21, 2007

Afrika Mashariki sarafu moja 2012



MARAIS wa nchi za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC) jana walikubaliana kuwa na sarafu moja na soko la pamoja kwa nchi za jumuiya hiyo ifikapo mwaka 2012.

Sambamba na uamuzi huo marais hao pia wamesogeza mbele uamuzi wa uharakishwaji wa kuanzishwa kwa Shirikisho la Afrika ya Mashariki.

Akisoma taarifa ya pamoja ya Marais hao mara baada ya kumalizika kwa mkutano wao katika Hoteli ya Ngurdoto jana, Katibu Mkuu EAC, Balozi Juma Mwapachu alisema wakuu hao wamefikia maamuzi hayo kutokana na maoni yaliyotolewa na wananchi wa nchi hizo na pia kuingizwa kwa Rwanda na Burundi kwenye jumuiya hiyo. Bonyeza hapa usome habari hii kwa kina katika gazeti letu la Mwananchi

No comments:

RAIS SAMIA ASHIRIKI NA KUTUNUKU TUZO ZA WASANII WA KOMEDI TANZANIA 2025

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameshiriki kama mgeni rasmi katika hafla ya utoaji wa Tuzo za Wasa...