Monday, August 06, 2007

Mshiriki wa Big Brother 2 mtanzania huyu hapa



Kama akishinda donge nono la dola za Marekani 100 000, Mtanzania, Richard Buzidenhout anasema atazitumia kununua vifaa vya kupigia picha za filamu . Mwakilishi huyo wa Big Brother kutoka Tanzania, mwenye umri wa miaka 24 na mwanafunzi wa fani ya filamu ana matarajio makubwa ya kuwa mtaalamu mahiri katika fani ya filamu na binafsi anamhusudu sana mtengenezaji filamu, Peter Jackson kwa umahiri wake.

Richard ambaye ni mshiriki pekee wa shindano hilo aliyeoa anasema kuwa anatamani sana kutembelea nyumbani kwao mkewe huko nchini Canada katika mji wa Brandon uliopo katika jimbo la Manitoba, Canada kushuhudia sehemu aliyokulia mkewe.

Anajielezea kama mtu anayependa mzaha, na kwamba ni mgumu sana kukasirishwa, lakini anasema tabia yake moja inayokera ni usumbufu na kelele nyakati za alfajiri, kabla wengi hawajaamka.

Anapanga kushinda Shindano hilo la Big Brother Africa 2 bila kushusha hadhi yake. Anapenda mazingira asili ya Afrika Mashariki, anasema kitu kinachomvutia zaidi ni kuendesha gari kupitia kreta ya Ngorogoro huku akishuhudia wanyama pori mbalimbali. 

Pia anasema eneo analolihusudu kulitembelea ni Serengeti na maeneo ya Pwani hasa Zanzibar.

Tafadhalini Watanzania tumpigieni kura Richard ili aweze kushinda kitita na hatimaye kupandisha chati Tanzania kimataifa.

Bonyeza hapa au Bonyeza hapa

Ukitaka kumuona cheki Richard hebu Bonyeza hapa

wengine wanaoshiriki Big Brother Africa ni hawa



Bertha Miaka: 28 Nchi: Zimbabwe Mji anaotoka: Harare Kazi: Mwanasheria/mshauri wa Uhusiano na mawasiliano.



Code Sangala Miaka: 31 Nchi: Mali Mji anaotoka: Blantyre Kazi: Mtangazaji/ DJ



Jina Jeff Miaka: 23 Nchi: Kenya Mji anaotoka: Kisumu Kazi: mtunzi wa vitabu, mshauri na mjasiliamali



Justice Motlhabani Miaka: 23 Nchi: Botswana Mji anaotoka: Serowe Kazi: Mwandishi wa kujitegemea/Mwanafunzi




Kwaku Miaka: 30 Nchi: Ghana mji anaotoka: Kumawu Kazi: Mjasiliamali.



Lerato Miaka: 23 Nchi: Afrika Kusini Mji anaotoka: Soweto Kazi: Mratibu wa matukio



Maureen Miaka: 27 Nchi: Uganda Mji anaotoka: Entebbe Kazi: Mbunifu wa mitindo




Maxwell Miaka: 26 Nchi: Zambia Mji anaotoka: Lusaka Kazi: Opareta wa simu



Meryl Miaka: 21 Nchi: Namibia Mji anaotoka: Windhoek Kazi: Mhudumu wa Mapokezi



Ofunnekama Miaka: 29 Nchi: Nigeria Mji anaotoka: Lagos Kazi: Katibu Muhtasi.



Tatiana Miaka: 26 Nchi: Angola Mji anaotoka: Luanda Kazi: Msanii/mwanamitindo

 

No comments: