Tuesday, August 07, 2007

Mshiriki wa Tanzania ana aibu

Kila suala analoulizwa jibu ni my wife, my wife, my wife, hawezi kujibu swali bila ya kumtaja mkewe... kama vile ni wa kwanza kuoa duniani, mdau Masaki kaligusia hili.

Suala hili linamfanya aanze kuonekana kama mtu anayeboa kuliko wote ndani ya nyumba, hata Watanzania nadhani wanaweza kuchoshwa na hali hii inabidi abadilike. Anatajwa mara chache mno na umaarufu wake miongoni mwa wenzie uko chini.

Katika siku yao ya pili, alfajiri mameti wa jumba la Big Brother wanaonekana kuondokewa na ujasiri waliokuwa nao siku ya jana walipokuwa wakiingia ndani ya jumba hilo, sababu Big Brother tayari keshawapiga mkwara mzito.

Wakati wa kuoga asubuhi ya leo kuna mambo kadhaa yalichomoza kuhusiana na joto la maji ya kuoga. Mameti wanagundua haraka kwamba kuna ujanja alioucheza Big Brother.

Meryl kwa mara nyingine tena anafanya kituko anavua nguo na kubakia mtupu, katika tukio hilo anafuatiwa na Tatiana, ambaye anaonekana kujawa na aibu tele kuonyesha mwili wake.

Pamoja na kuinyesha utundu na mara kadhaa kuwa karibu sana na wanaume,
, Lerato anaamua kuoga na nguo yake. Inawezekana hii ni mbinu yake ya kuwatia kiu mashabiki wake ili kusudi wawe na uchu wa kuona mwili wake.

No comments: