Saturday, December 14, 2024

DR. KEDMON MAPANA ATEMBELEA BANDA LA NHC!






Leo, Katibu Mtendaji wa BASATA, Dr. Kedmon Mapana, ametembelea banda la National Housing Corporation (NHC) kwenye Tamasha la Kimataifa la Maendeleo ya Filamu na Sanaa linaloendelea viwanja vya Posta, Dar es Salaam! 🎬🏠

Dr. Mapana amepongeza juhudi za NHC katika kuboresha maisha ya Watanzania kupitia miradi ya makazi ya kisasa na fursa za uwekezaji. Amesisitiza pia jinsi sanaa na sekta ya ujenzi zinavyoweza kushirikiana kuchochea maendeleo ya uchumi wa taifa! 🌍💡

Njoo na wewe! Tembelea banda la NHC ujionee fursa za kumiliki nyumba bora, ofisi za kisasa, na maeneo ya kibiashara kwa gharama nafuu. Hii ni nafasi yako ya kutimiza ndoto zako za makazi bora!

📍 Viwanja vya Posta, Dar es Salaam

👉 #MaishaNiNyumba #NHCTanzania #TamashaLaSanaa #FursaZaMakazi #KujengaNdoto #InvestInYourFuture


No comments:

RAIS SAMIA ASHIRIKI NA KUTUNUKU TUZO ZA WASANII WA KOMEDI TANZANIA 2025

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameshiriki kama mgeni rasmi katika hafla ya utoaji wa Tuzo za Wasa...