Saturday, December 14, 2024

DR. KEDMON MAPANA ATEMBELEA BANDA LA NHC!






Leo, Katibu Mtendaji wa BASATA, Dr. Kedmon Mapana, ametembelea banda la National Housing Corporation (NHC) kwenye Tamasha la Kimataifa la Maendeleo ya Filamu na Sanaa linaloendelea viwanja vya Posta, Dar es Salaam! 🎬🏠

Dr. Mapana amepongeza juhudi za NHC katika kuboresha maisha ya Watanzania kupitia miradi ya makazi ya kisasa na fursa za uwekezaji. Amesisitiza pia jinsi sanaa na sekta ya ujenzi zinavyoweza kushirikiana kuchochea maendeleo ya uchumi wa taifa! 🌍💡

Njoo na wewe! Tembelea banda la NHC ujionee fursa za kumiliki nyumba bora, ofisi za kisasa, na maeneo ya kibiashara kwa gharama nafuu. Hii ni nafasi yako ya kutimiza ndoto zako za makazi bora!

📍 Viwanja vya Posta, Dar es Salaam

👉 #MaishaNiNyumba #NHCTanzania #TamashaLaSanaa #FursaZaMakazi #KujengaNdoto #InvestInYourFuture


No comments:

NAIBU WAZIRI WA FEDHA AMWAKILISHA WAZIRI WA FEDHA KATIKA KONGAMANO LA 16 LA MWAKA LA WATAALAM WA UNUNUZI NA UGAVI – ARUSHA

Naibu Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Mhandisi Mshamu Ali Munde, amemwakilisha Waziri wa Fedha katika ufunguzi wa Kongamano la 16 la Mwaka la Wa...