Saturday, December 28, 2024

AJALI YA GARI YAUA WATU SITA NYASA,WAMO WALIMU WANNE

 


Watu sita wamefariki dunia katika ajali ya gari iliyotokea katika Wilaya ya Nyasa, Mkoani Ruvuma
Ajali hiyo imetokea leo, tarehe 28 Desemba 2024, wakati wa safari kutoka kijiji cha Lumalu kilichopo katika Kata ya Upolo kuelekea makao makuu ya wilaya.
Akizungumza kwa njia ya simu, Mkuu wa Wilaya ya Nyasa, Mheshimiwa Peres Magiri, amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo, ambayo imesababisha vifo vya wafanyakazi wanne wa Serikali, wakiwa ni walimu wa Shule ya Msingi Lumalu.
Watu wawili wengine, wakiwemo dereva wa gari hilo na raia mmoja, pia amepoteza maisha.
Gari lililohusika katika ajali hiyo ni la aina ya Prado T 647 CVR, mali ya Vincent Alel Milinga kutoka kijiji cha Lumalu, Kata ya Upolo, Wilaya ya Nyasa.
Walimu waliopoteza maisha ni Damas Damasi Nambombe (Mwalimu),Domenica Abeat Ndau (Mwalimu),Judith Joseph Nyoni (Mwalimu),na John Silvester Mtuhi (Mwalimu).
Raia mwingine aliyefariki duni ni Boniface Bosco Mapunda pamoja na dereva wa gari hilo ambaye ni Vincent Alel Milinga.



 

No comments:

TARURA MUSOMA WAPONGEZWA UJENZI WA MIRADI KULINGANA NA THAMANI YA FEDHA

  Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Ndugu Ismail Ali Ussi amewapongeza wafanyakazi wa TARURA wilaya ya Musoma kwa kufanya kazi kwa weledi n...