Thursday, June 22, 2017

ZIARA YA RAIS DK. MAGUFULI MKOA WA PWANI, AZINDUA MIRADI UKIWEMO WA MAJI WA RUVU JUU

Rais Dk. John Magufuli akilijaribu kuliwasha Trekta katika kiwanda cha kutengeneza  matrekta ya URSUS kilichopo Kibaha mkoani Pwani, wakati akizindua Kiwanda hicho, akiwa katika ziara ya siku tatu katika mkoa wa Pwani, jana.
Rais Dk. John Magufuli akifungua kiwanda cha kutengeneza  matrekta ya URSUS kilichopo Kibaha mkoani Pwani, jana.
Rais Dk. JohnMagufuli akiweka jiwe la msingi kwenye sehemu ya kiwanda cha kutengeneza  matrekta ya URSUS kilichopo Kibaha mkoani Pwani. 
 Rais Dk. John Magufuli akizungumza jambo na Waziri wa Viwanda na Biashara Charles Mwijage kabla ya kufungua kiwanda cha Nondo cha Kilua Steel Group kilichopo Mlandizi mkoani Pwani, jana.
 Rais Dk. John Magufuli  akipeperusha bendera kuashiria kuiruhusu treni ya TRL kusafirisha nondo kutoka kwenye kiwanda cha Nondo cha Kilua Steel Group kilichopo Mlandizi mkoani Pwani, jana.
 Rais Dk. John Magufuli   akishirikiana  na viongozi wengine kukata utepe wakati akifungua kiwanda hicho cha nondo. 
 Rais Dk. John Magufuli akishirikiana na Waziri wa Maji Mhandisi Gerson Lwenge, Balozi wa India hapa Nchini Sandeep Arya, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Humphrey Polepole (kushoto),  na Viongozi wengine wa Mkoa wa Pwani na Serikali kukata utepe kuzinduzi rasmi wa Mradi Mkubwa wa Maji wa Ruvu Juu Mlandizi Mkoani Pwani, jana.
 Rais Dk. John Magufuli akimpongeza Waziri wa Maji Mhandisi Gerson Lwenge baada ya kuzindua rasmi Mradi wa upanuzi wa Mitambo ya kusafisha maji Ruvu juu Mlandizi Mkaoni Pwani.
 Rais Dk. John Magufuli akisalimiana na Mtendaji Mkuu wa DAWASA Mhandisi Archard Mutalemwa  baada ya kuzindua mradi huo Mkubwa wa maji
 Rais Dk. John Magufuli akiangalia hatua za usafishaji wa maji katika kituo cha kusafisha maji cha Ruvu juu Mlandizi Mkoani Pwani, kushoto ni Mtendaji mkuu wa DAWASCO Mhandisi Cyprian Luhemeja akitoa maelezo
 Rais Dk. John Magufuli akishirikiana na Balozi wa India hapa nchini Sandeep Arya kupiga ngoma, baada kuzindua mradi huo mkubwa wa kusafisha na kuzalisha Maji kwa ajili ya miji ya Pwani na Dar es Salaam.
 Rais Dk. John Magufuli akiangalia ujumbe aliotumiwa kwa njia ya mdandao na Waziri Mkuu wa India Narendra Modi kupitia Luninga kabla ya kuzindua Mradi huo wa maji
 Rais Dk. John Magufuli akihutubia kabla ya kuzindua Mradi huo wa maji wa Ruvu juu Mlandizi mkoani Pwani.
 Sehemu ya Mradi huo wa maji wa Ruvu juu Mlandizi Mkoani Pwani
 Rais Dk. John Magufuli akiangalia Mfuko wa sandarusi kabla ya kuzindua kiwanda cha Global Packing kilichopo Kibaha mkoani Pwani. PICHA ZOTE NA IKULU.

No comments: