Thursday, June 22, 2017

OFISI YA MANISPAA YA ILALA YAHAMIA KWA MUDA VIWANJA VYA MNAZI MMOJA KUWAHUDUMIA WANANCHI KATIKA KUADHIMISHA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA

 Mkuu wa Wilaya ya Ilala , Sophia Mjema akizungumza na mmoja wa wazee waliofika kupatiwa huduma katika viwanja vya Mnazi Mmoja ambapo ofisi nzima ya Manispaa hiyo imehamia viwanjani hapo kwa ajili ya kuhudumia watu ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma katika wilaya hiyo.
 Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilala , Edward Mpogolo akiwa na Naibu Meya wa Manispaa hiyo Omary Kumbilamoto wakitoa huduma kwa wadau waliofika kutaka msaada juu ya mambo yanayowakabili . Ofisi za Manispaa hiyo zimahamia hapo kwa muda kwa ajili ya kuhudumia watu, ikiwa ni sehemu ya mahadhimisho ya wiki ya utumishi wa Umma katika wilaya hiyo.
Mkurugenzi  wa Manispaa ya Ilala Msongela Palela akimuhudumia mmoja wa wakazi wa jiji la Dar es Salaam waliofika katika viwanja vya mnazi mmoja.
  Mkuu wa Wilaya ya Ilala , Sophia Mjema akipata maelezo kutoka kwa mmoja wa wakilishi wa kampuni ya kuuza vifaa vya kuzimia moto inayojulikana kwa jina la Zima Moto  
 Afisa mkaguzi  Msaidiz wa jeshi la Zima Moto , akitoa maelezo kwa  Mkuu wa Wilaya ya Ilala , Sophia Mjema wakati wa maonyesho ya wiki ya utumishi wa Umma yaliyofanyika katika Viwanja vya mnazi mmoja Dar es Salaam.
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala , Sophia Mjema akizungumza na baadhi ya watumishi wa Manispaa ya Ilala ambo wanatoa huduma kwa wananchi katika Viwanja vya mnazi mmoja 

No comments: