Tuesday, September 21, 2010

Rais Kikwete ahudhuria msiba wa Julius Msekwa


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini katika kitabu cha maombolezo wakati alipokwenda kuifariji familia ya Marehemu Julius Msekwa ambaye ni mtoto wa Makamu mwenyekiti wa CCM Bara Pius Msekwa nyumbani kwao Bongoyo Oysterbay, jijini Dar es Salaam jana jioni.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitoa heshima za mwisho kwa marehemu Julius Msekwa ambaye ni mtoto wa Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Pius Msekwa wakati wa ibada ya mazishi iliyofanyika nyumbani kwa wazazi wa marehemu , Bongoyo Oysterbay jijini Dar es Salaam jana jioni. Marehemu Julius Msekwa aliyefariki wiki iliyopita huko Nicosia Cyprus ambapo alikuwa akifanya kazi ya mtaalamu Mshauri bingwa katika fani ya teknolojia ya Mawasiliano, alizikwa jana katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete,(wapili kushoto) Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Pius Msekwa(kushoto) na mkewe Mama Anna Abdallah (watatu kushoto) pamoja na Rais mstaafu awamu ya tatu Mzee Ali Hassan Mwinyi (kulia) wakishiriki ibada ya mazishi ya kumuombea Marehemu Julius Msekwa aliyefariki huko Nicosia Cyprus wiki iliyopita na kuzikwa jana katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.(picha zotena Freddy Maro).

1 comment:

Anonymous said...

huyu jamaa msekwa kama unavyojua wameuza nchi kusaidia familia zao, jiulize kwa nini mwanae kafia nje, kama alivyosema Malcom X ikifika jioni vifaranga hurudi nyumbani na mama, mungu anamwonyesha dhuluma zake!!!!!