Monday, September 20, 2010

Ethiopian Airways yapata bosi mpya


BODI ya uendeshaji wa Shirika la ndege ya Ethiopian Airlines imeteua Ato Tewolde G. Mariam kuwa Afisa Mtendaji Mkuu wa shirika hilo.

Tewolde ambaye kwa kipindi kirefu amekuwa katika nyadhifa mbalimbali katika shirika hilo, na kuendesha ofisi mbalimbali za shirika hilo duniani ikiwemo India, Saudi Arabia na Marekani anachukua nafasi ya Ato Gilma Ako kuanzia Januari 2011.

Mbali na nafasi hizo Tewolde alikuwa Afisa Mtendaji wa Masoko na mauzo wa Ethiopian Airlines na anaelezwa na Mwenyekiti wa bodi kuwa aliweza kukuza faida ya shirika hilo na kuliwezesha kuwa shuirika linalojiweza Afrika.

Taarifa iliyotolewa na Mwenyekti wa Bodi hiyo, Ato Seyoum Mesfin imeeleza kuwa imempongeza Ato Girma wake kwakuwweza kuendesha shirika hilo kama Afisa mtendaji Mkuu tokea mwaka 2004 na kufanya shirika kukua na kujenaga heshima kwa kipindi chote hicho.

“Ato Girma amewezesha shirika kukuwa katia historia la Shirika kutokana na Mpango 2010 uliowezesha shirika hilo kuwa la 16 katika mashirika yanayopata faida duniani”.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa imechukua uamuzi huo ili kuwezesha shirika hilo kutekeleza kikamilifu mpango wa 2025 ambapo linahitaji kujitanua zaidi na hivyo kuteua mtu anayefaa kuweza kuendesha shirika hjilo wakati Ato Girma anastaafu.

“Kwa kuwa atio Girma amefanya kazi kwa muda wa miaka 37 , muda umefika kwake kustaafu na Ato Tewolder Gebremariam ameteuliwa kama Mtendaji Mkuu mteule mpaka Desemba 2010 kabla ya kuanza kazi rasmi”.

1 comment:

zitto kiaratu said...

keep up the good work, you re pride of africa, if there is anything run with integrity in africa it is Ethiopian Airlines, you even provide training for your fellow africans in mechanics, avionics etc " going great length to please"