Monday, September 20, 2010

Kampeni za vyama vingine bwana!!!


Katibu Mkuu wa chama cha Alliance for Tanzania Farmers Party Rashid Ligania Rai (kulia) akimnadi mgombea urais wa Zanzibar kupitia chama hicho, Said Soud kwenye uzinduzi wa kampeni za chama hicho cha wakulima kwenye uwanja wa Komba wapya mjini Zanzibar jana.

Wamasai waliohudhuria mkutano wa uzinduzi wa kampeni za chama cha wakulima cha, Alliance for Tanzania Farmers Party ambapo mgombea urais wa Zanzibar wa chama hicho, Said Soud amelaani tabia ya uongozi wa baraza la manispa la kuwanyanyasa wamasai wanaofanyabiashara kwenye mji wa Zanzibar.

3611: Mgombea Urais wa zanzibar kupitia chama ca Alliance for Tanzania Farmers Party, Said Soud (kushoto) akiteta jambo na Katibu Mkuu wa chama hicho, Rashid Ligania Rai wakati wa uzinduzi wa kampeni za chama hicho kwenye uwanja wa Komba wapya mjini Zanzibar jana. Picha zote na Martin Kabemba.

No comments: