Saturday, December 02, 2006

Mkutano wa TED Global kufanyika Tanzania


MKUTANO mkubwa duniani wa kila mwaka wa masuala ya teknolojia, (technology, entertaiment, design) unaowashirikisha watu maarufu duniani wanaozidi 1000, utafanyika Tanzania kwa mara ya kwanza.

Akitangaza rasmi jana jijini hapa New York, Mkurugenzi wa Programu wa TED, Emeka Okafor (pichani kushoto), Emeka unaweza kumfikia kwa kubonya hapaalisema mkutano huo umeamuliwa kufanyika rasmi Tanzania kutokana na mafanikio makubwa iliyoyapata Tanzania katika nyanja mbalimbali ikiwamo uchumi na siasa.

“Hatujaichhagua Tanzania kwa bahati mbaya au kwa upendeleo tu, au eti tunataka kutazama wanyama wa mbugani, la hasha , bali ni kwasababu ya mafanikio makubwa nchi hiyo iliyoyapata kiuchumi na kisiasa,”alisema Okafor.

Kama wewe unajihusisha na masuala ya teknolojia na biashara, tuma maombi yako ili uweze kuhudhuria mkutano huu. Watu utakaokutana nao ana na mada zinazojadiliwa kwenye mikutano ya TED, utasuuzika nafsi yako.

No comments: