Sunday, January 04, 2026

BILIONI 37.7 ZATIKISA TANGA: TARURA YASUKUMA MAPINDUZI YA BARABARA






MAMLAKA ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) mkoa wa Tanga imepiga hatua kubwa katika utekelezaji wa miradi ya miundombinu ya barabara, ambapo asilimia 80 ya miradi ya mwaka wa fedha 2024/2025 tayari imekamilika.

Akizungumza katika mahojiano maalum, Meneja wa TARURA mkoa wa Tanga, Mhandisi George Tarimo, amesema kuwa asilimia 20 iliyosalia ya miradi ipo katika hatua za mwisho na inatarajiwa kukamilika kwa mujibu wa ratiba zilizopangwa.

Mhandisi Tarimo amesema mafanikio hayo yametokana na usimamizi mzuri wa miradi pamoja na kuimarika kwa upatikanaji wa fedha, akibainisha kuwa katika miaka ya nyuma TARURA ilikuwa ikitegemea zaidi Mfuko wa Barabara (Road Fund) kama chanzo kikuu cha ufadhili.

Akizungumzia mwaka wa fedha wa sasa 2025/2026, Mhandisi Tarimo amesema TARURA tayari imeanza utekelezaji wa miradi mipya, ambapo miradi 28 imeshakabidhiwa rasmi kwa wakandarasi kwa ajili ya utekelezaji.

Ameongeza kuwa kwa ujumla, miradi 125 ya barabara inatarajiwa kutekelezwa katika mkoa wa Tanga ndani ya mwaka huu wa fedha, hali inayoonesha ongezeko kubwa la bajeti na wigo wa miradi ikilinganishwa na miaka mitano iliyopita.

Kwa mujibu wa Mhandisi Tarimo, jumla ya shilingi bilioni 37.7 zimetengwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya miundombinu ya barabara mkoani Tanga kwa mwaka wa fedha 2025/2026.

Amesema fedha hizo zimetokana na vyanzo vitatu vikuu ambavyo ni Shilingi bilioni 13.2 kutoka Mfuko wa Barabara (Road Fund), Shilingi bilioni 6.5 kutoka Fedha za Maendeleo ya Majimbo, Shilingi bilioni 7.4 kutoka tozo ya mafuta.

Pia Amesema kuongezeka na kutofautishwa kwa vyanzo vya fedha kumeimarisha uwezo wa TARURA kutekeleza miradi mingi kwa wakati mmoja na kupunguza utegemezi wa chanzo kimoja cha fedha.

Mhandisi Tarimo ameongeza kuwa TARURA inaendelea na ukarabati wa miundombinu ya barabara licha ya changamoto ya baadhi ya miundombinu hiyo kuharibiwa kwa makusudi na watu wenye nia ovu.

Ametaja taa za barabarani kuwa miongoni mwa maeneo yaliyokuwa yakichangia gharama kubwa za matumizi ya umeme, hali iliyosababisha TARURA kuanza kubadilisha taa za umeme wa kawaida na kuweka taa zinazotumia nishati ya jua (solar).

 Zoezi hilo tayari limeanza katika baadhi ya maeneo na litaendelea sambamba na miradi ya sasa na ijayo ya ukarabati wa barabara katika mkoa huo.

Aidha, Mhandisi Tarimo aliendelea kusema TARURA inaendelea kutekeleza mkakati maalum unaoendana na sera ya umiliki wa asilimia 30 kwa wananchi, unaolenga kuwawezesha wakazi wa maeneo husika kushiriki kikamilifu katika matengenezo ya miundombinu ya barabara.

Mkakati huo unatekelezwa kupitia mpango wa Community-Based Routine Maintenance, unaowawezesha wananchi kufanya matengenezo madogo ya barabara na kulipwa kwa kazi hiyo.

Mpango huo unatarajiwa kuanza awali katika maeneo ya Korogwe, Lushoto na Pangani, ambako tayari kuna vikundi vya wananchi vilivyosajiliwa, na unalenga pia kuzalisha ajira na kuimarisha umiliki wa miundombinu kwa wananchi.

Mhandisi George Tarimo amewahimiza wananchi wa mkoa wa Tanga kulinda na kutunza miundombinu ya barabara, akisisitiza kuwa utunzaji wa rasilimali za umma ni nguzo muhimu katika kuharakisha maendeleo endelevu ya kijamii na kiuchumi ya mkoa huo.

RAIS MWINYI: SMZ KUENDELEA KUJENGA MASOKO YA KISASA KATIKA KUIMARISHA BIASHARA ZANZIBAR.












Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Serikali itaendelea na ujenzi wa masoko ya kisasa katika maeneo mbalimbali ya Zanzibar kwa lengo la kuwawezesha wafanyabiashara kufanya shughuli zao katika mazingira bora, salama na yenye hadhi.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 4 Disemba 2026 alipolizindua Soko la Kisasa la Mbogamboga la Mombasa, lililopo Mkoa wa Mjini Magharibi.

Ameeleza kuwa Serikali inapowahamisha wafanyabiashara kutoka maeneo yao ya awali, hufanya hivyo kwa nia njema ya kujenga masoko yenye viwango na hadhi, pamoja na kuwaandalia mazingira mazuri yatakayochangia ukuaji wa biashara zao na ustawi wa maisha yao.

Rais Dkt. Mwinyi amewahakikishia wananchi kuwa Serikali ipo katika maandalizi ya kujenga soko kubwa na la kisasa katika eneo la Kibanda Maiti, pamoja na uanzishaji wa Bazaar katika Mtaa wa Kwa Hajitumbo, Wilaya ya Mjini, hatua itakayosaidia kudhibiti biashara holela, kuondoa mazingira duni katika masoko na kuzuia ufanyaji wa biashara pembezoni mwa barabara.

Aidha, amesema Serikali itaendelea kutoa mikopo isiyo na riba kwa wafanyabiashara ili kuwawezesha kukuza mitaji yao, huku akitoa wito kwa watakaopewa fursa ya kuliendesha soko hilo jipya kuhakikisha wanalinda miundombinu na kuimarisha usafi wakati wote.

Rais Dkt. Mwinyi ametoa maelekezo maalum kwamba wafanyabiashara wa mwanzo waliopisha ujenzi wa Soko la Mombasa wapewe kipaumbele wakati wa ugawaji wa vizimba vya kufanyia biashara sokoni hapo.

Vilevile, ameushauri Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (ZSSF) kujikita zaidi katika uwekezaji wa miradi mikubwa yenye tija, ikiwemo nishati ya umeme, teksi za baharini na mabasi ya umeme, kufuatia mafanikio yaliyopatikana katika miradi ya nyumba za Makaazi na Masoko.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF), Ndugu Nassor Shaaban, ameishukuru Serikali kwa kuendelea kuiamini taasisi hiyo katika utekelezaji wa miradi ya uwekezaji inayochangia ukuaji wa uchumi na maendeleo ya Zanzibar, ikiwemo ujenzi wa nyumba za Makaazi na Masoko ya kisasa.

Ujenzi wa Soko la Kisasa la Mbogamboga la Mombasa umegharimu jumla ya Shilingi Bilioni 16.6, na umetekelezwa na Kampuni ya RANS

ARUSHA NATIONAL PARK RANKED THIRD AMONG 20 BEST PLACES TO VISIT IN 2026 - CNN TRAVEL







By Philipo Hassan

Arusha National Park, found in Arusha, Tanzania was mentioned by CNN Travel in their latest article published on December 31, 2025 recognizing not only the park but the entire Arusha region as one of the best places to travel in 2026. The report highlights Arusha for its vibrant cultural developments, natural beauty, and unique safari experiences, placing it high on the global travel radar for the year of 2026.

Arusha is a gateway to most of Africa’s most iconic attractions, including Mount Kilimanjaro, Serengeti National Park, Tarangire National Park, Lake Manyara National Park, and Ngorongoro Conservation Area, making it a favorable place for visitors exploring northern tourism destinations.

CNN Travel writes of Arusha that “At the foot of imposing volcanic Mount Meru lies the city of Arusha, in Tanzania, in the east of Africa. Not far from the wildlife filled Serengeti National Park and close to base camp for Mount Kilimanjaro, Arusha is often a gateway to other adventures.” 

The article highlights Arusha National Park as a key attraction in the region, with visitors also able to explore Serengeti, Tarangire, Lake Manyara, and the Ngorongoro Conservation Area, offering unforgettable wildlife encounters and breathtaking experiences.

Within Arusha National Park itself, travelers can enjoy a remarkable range of attractions, from game drives past roaming giraffes and elephants to flamingo studded alkaline lakes like Momella, as well as lush forest and mountain scenery on the slopes of Mount Meru. The park’s varied landscapes and wildlife encounters offer a unique complement to the wider northern safari circuit.

CNN Travel lists other top destinations to visit in 2026, including Adelaide (Australia), Algeria, Aragon (Spain), Bahrain, Brussels (Belgium), the Chilean fjords, Devon (UK), Dominica, East Timor, Jamaica, Kanazawa (Japan), Orkhon Valley (Mongolia), Oulu (Finland), Penang (Malaysia), PeƱico (Peru), Philadelphia (USA), Sail250 events along the US East Coast, Santa Monica (California, USA), and St. Pierre and Miquelon (France), showcasing a diverse range of cultural, historical, and natural experiences around the world that travelers should explore in this year

DKT. JAKAYA KIKWETE AONGOZA UZINDUZI WA JENGO LA UHAMIAJI PEMBA KATIKA MAADHIMISHO YA MIAKA 62 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

Rais Mstaafu Awamu ya Nne wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete, akiwasili Kisiwani Pemba kwa ajili ya Sherehe ya Uzinduzi wa Jengo la Afisi ya Uhamiaji na Makaazi ya Askari,Wilaya ya Micheweni, mkoa wa Kaskazini Pemba, ambapo amepokelewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dkt. Anna Makakala na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Mgeni Hassan Yahaya. Uzinduzi huo ni sehemu ya Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar.Uzinduzi huo utafanyika leo,tarehe 4 Januari,2026.



Pemba, Zanzibar | Januari 4, 2026

Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, amewasili kisiwani Pemba kwa ajili ya Sherehe ya Uzinduzi wa Jengo la Ofisi ya Uhamiaji pamoja na Makazi ya Askari, tukio muhimu linalofanyika Wilaya ya Micheweni, Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Mara baada ya kuwasili, Dkt. Kikwete amepokelewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Anna Makakala, pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba, Mgeni Hassan Yahaya.

Uzinduzi wa jengo hilo unafanyika leo tarehe 4 Januari, 2026, na ni sehemu ya Maadhimisho ya Miaka 62 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, yanayoendelea kuenzi historia, mshikamano na maendeleo ya wananchi wa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.

Jengo hilo jipya la Ofisi ya Uhamiaji na Makazi ya Askari linatarajiwa kuimarisha utoaji wa huduma za uhamiaji, kuongeza ufanisi wa kiutendaji pamoja na kuboresha mazingira ya kazi na makazi kwa askari, hatua inayochochea usalama, utulivu na maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Ushiriki wa Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete katika uzinduzi huu unaendelea kuakisi mshikamano wa kitaifa, kuthamini mchango wa viongozi waliotangulia na kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuimarisha miundombinu na huduma muhimu kwa wananchi, hususan katika kipindi hiki cha maadhimisho ya kihistoria ya Mapinduzi ya Zanzibar.

BILIONI 37.7 ZATIKISA TANGA: TARURA YASUKUMA MAPINDUZI YA BARABARA

MAMLAKA ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) mkoa wa Tanga imepiga hatua kubwa katika utekelezaji wa miradi ya miundombinu ya baraba...