Tuesday, June 22, 2010

Mhadiri Suza ang'ara kimataifa



MHADHIRI wa chuo cha SUZA, Dk Mohammed Ali Sheikh, anayefundisha somo la kemia, ametajwa kuwa miongoni mwa wanasayansi mia duniani wa mwaka 2010.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jijini Dar es Salaam kutoka katika taasisi ya kimataifa ya "Biographical Centre "(IBC),ilieleza kuwa mhadhiri huyo anayefundisha somo hilo ametajwa kuwa miongoni mwa wanasayansi bora duniani.

ilieleza kuwa Kila mwaka taasisi hiyo inatangaza wanasayansi bora 100 ambao wanapatikana duniani, kwa somo la sayansi ambao wanapatikana kwa njia ya utafiti maalumu wa kina.

"IBC inaamini kuwa utafiti huu unalengo la kuwavutia wanasayansi mbalimbali wa mjini, na vijijini hata wa kimataifa kwa bila ya kupendelea jinsia ambao wametoa mchango wa kutosha katika elimu ya sayansi,hivyo Dk Sheikh anavyo vigezo hivyo na sasa ni mwanachama wa IBC," alisema sehemu ya taarifa hiyo.

Sehemu ya taarifa hiyo pia ilisema kuwa Dk Sheikh anaongoza kitengo cha biashara na ushauri wa taaluma katika chuo cha Suza.

Kwa sasa Dk Sheikh amekuwa mwanachama wa wanasayansi mbalimbali wa taaluma na jumuiya ya wanasayansi, ambazo ni pamoja na jumuiya ya Kijapan ya mazingira na kemia, afya na uongozi ya Canada, teknolojia ya majini, iliyopo nchini Canada,Jumuiya ya kimatiafa ya mazingira na uchambuzi wa kemia,umoja wa elimu ya fizikia ya dunia, na elimu ya sayansi ya dunia.

No comments: