Wednesday, June 23, 2010

Kinara wa mihadarati akamatwa Jamaica


Christopher Dudus jambazi sugu wa mihadarati Jamaica
Polisi nchini Jamaica wamemkamata kiongozi sugu wa biashara za mihadarati nchini humo Christopher Dudus Coke viungani mwa mji mkuu, Kingston.

Bwana Coke ambaye amekuwa akisakwa kwa muda mrefu, anatakiwa nchini Marekani kwa mashtaka ya ulanguzi wa dawa za kulevya pamoja na biashara haramu za silaha.

Juhudi za kumkamata Coke mwezi jana zilisabisha vurugu nchini humo ambapo watu zaidi ya sabini waliuawa.

Mkuu wa polisi nchini Jamaica, Owen Ellington, alisema kuwa maafisa wake wa polisi wameonywa dhidi ya kutokea vurugu zingine kufuatia kukamatwa kwa bwana Coke.

Huenda akafikishwa mahakamani katika muda wa masaa arobaini na nane.

Bwana Coke alitajwa kama mmoja wa majambazi sugu zaidi duniani, ingawa wafuasi wake wanasema yeye ni kiongozi wa jamii.

1 comment:

Anonymous said...

tatizo hapa sio huyu jamaa isipokuwa wamarekani ambao wanataka hiyo cocaine, huyu jamaa anahudumia wateja wake ambao wanataka madawa haramu(addicted americans) inatakiwa wamarekani wachunge mipaka yao wazuie hayo madawa kufikia raia zao, wanajifanya raia zao hawana makosa, isipokuwa huyu jamaa ndio mhalifu, we are puppets of americans, supposed to do whatever they ask us to do, then again look e.g. guinea never had any election in 52 years, bongo hatujawahi kuwa na uchaguzi wa haki tangu wakoloni watupe uhuru!!!!