Thursday, June 24, 2010

Jaji Mkuu aapisha mawakili 128


Mke wa Rais Mama salma Kikwete, akimpongeza mwanae, Ridhiwani Kikwete, kwa kumpa shada la maua baada ya kutunukiwa Cheti cha kuwa Wakili wa kujitegemea, wakati wa hafla ya kuwatunuku mawakili 128, iliyofanyika kwenye viwanja vya Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam leo.






Jaji mkuu wa Tanzania Mh.Augustino Ramadhan leo amekabidhi hati za uwakili kwa mawakili 128 katika mahakama kuu jijini Dar es Salaam

Katika tukio hilo lililofanyika mapema leo tarehe 24 ambapo Mwenyekiti wa WAMA na mke mheshimiwa rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mama Salma Kikwete amehudhuria na kushuhudia zoezi zima la kupatiwa kwa hati mawakili hao.

Aidha katika zoezi hilo limeonesha kuwa ni la kufurahisha kwa familia ya rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kwa mtoto wake ambaye sasa ni wakili Ridhiwani Jakaya Mrisho Kikwete kuwa miongoni mwa mawakili waliotunukiwa hati hizo leo.

Katika sherehe hizo pia mawakili wa kujitegemea walifika kushuhudia tukio hilo ambapo walifurahishwa sana na wenzano kutokana na uvumilivu waliokuwa nao hata kufikia hatua ya kupata hati ya kuwa Wakili.

Pia wamewataka mawakili hao kutumia vizuri heshima waliyopewa ili kuepukana na kinachoisumbua serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania(Utumiaji mbovu wa madaraka na kutokutenda haki)kitendo ambacho kinaitesa jamii nzima ya Watanzania.

No comments: