Monday, June 21, 2010

Jk achukua fomu




RAIS Jakaya Kikwete jana alianza rasmi mbio za kutetea nafasi yake ya urais na kueleza kuwa vipaumbele vya serikali yake mpya vitasukumwa na misingi kumi, ikiwemo kuongeza kasi ya mapambano ya rushwa na matumizi mabaya ya madaraka.
Akihutubia mamia ya wakazi wa mji wa Dodoma muda mfupi baada ya kuchukua fomu ya kuomba ridhaa ya CCM kugombea urais, Rais Kikwete alisema vita dhidi ya rushwa itaenda sambamba na kuimarisha utawala bora, utawala wa sheria, demokrasia na mapambano ya ubadhirifu wa mali za umma.
“Nitatumia bidii yangu yote kufanya kampeni ya kukipigania chama chetu kipate ushindi mkubwa na mara tutakapofanikiwa, vipaumbele vya serikali ijayo vitasukumwa na misingi kumi ifuatayo,” alisena Rais Kikwete na kuongeza:
“Kuhakikisha kwamba nchi inaendelea kuwa na umoja, amani na usalama, Kujenga msingi wa uchumi wa kisasa wa Taifa linalojitegemea kwa kuchukua hatua madhubuti za kuharakisha zaidi mapinduzi ya kilimo, ufugaji, uvuvi na viwanda”
Alisema vipaumbele vingine ni kuongeza jitihada na mipango zaidi ya kuwawezesha kiuchumi wananchi hasa wa hali ya chini ili wawezze kushiriki na kunufaika na uchumi wwetu unaokua. Lakini vilevile tutaweka mkazo katiak ulitambua na kuliwezesha kwa namba yak kundi la wajasiriamali wa tabaka la kati ili waweze kushiriki katika uwekezaji mkubwa katika nchi yetu.

1 comment:

Anonymous said...

shamrashamra za bure hakuna uchaguzi wa haki hapa, bongo tutapata haki watu kama msekwa,ngombale mwiru, mkapa n.k. wakiaga dunia, hiyo itakuwa bahati nasibu ya wote.