Friday, December 25, 2009

Papa aangushwa chini na mwanamke



Sherehe za Krismasi mwaka huu kwenye makao makuu ya kanisa Katoliki huko Vatican zilitiwa dosari wakati Baba Mtakatifu alisukumwa chini na mwanamke.

Taarifa zasema mwanamke huyo ambaye jina lake halijulikani na ana matatizo ya akili amekamatwa na polisi.

Papa Benedict XVI alikuwa akijiandaa kuongoza misa maalum ya kusherehekea Krismasi wakati mwanamke huyo alivuka mpaka wa ulinzi.

Baba Mtakatifu hakuonyesha ishara zozote za kujeruhiwa kwa kuwa alinyanyuka huku akisaidiwa na msimamizi wa sherehe hizo.

Misa ya Krismasi mwaka huu iliandaliwa saa mbili kabla ya muda wa kawaida ili kumwezesha Papa kupumzika.

Taarifa zasema Askofu Mkuu Roger Etchegaray ambaye pia alisukumwa chini na mwanamke huyo alikimbizwa hospitalini kupimwa iwapo alijeruhiwa.

1 comment:

tathe said...

continue reading this click here for more address Discover More find more site link