Monday, January 05, 2009

Mboma: Kitambi kimeniangusha

ALIYEKUWA Mkuu wa Majeshi Nchini, Meja Jenerali, Robert Mboma, amesema anaamini kitambi alicho nacho kimesababisha kushindwa katika kura za maoni za Chama cha Mapinduzi (CCM) za ubunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini.

Mboma aliyasema hayo juzi wakati akiwashukuru wananchi katika uzinduzi wa kampeni za chama hicho za kinyang'anyiro cha ubunge wa jimbo hilo.

Alisisitiza kuwa anaamini kilichochangia kutopata kura nyingi zaidi ni kitambi
hicho alichokuwa nacho na kwamba hali hiyo itamkomaza kisiasa.

Mboma ambaye aliwashangaza baadhi ya watu walioshuhudia uzinduzi wa kampeni hizo uliofanywa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi katika kijiji cha Ilembo Mbeya vijijini. alisema kkuanguka kwake katika jimbo hilo kumetokana
na wananchama wa chama hicho kumnyima kura.Imeandikwa na Hawa Mathias kutoka Mbeya

No comments: