Sunday, January 11, 2009

Buriani Casian Malima




MWILI wa aliyekuwa Mhariri wa HabariLeo, Cassian Malima (44) utaagwa kesho na
kusafirishwa kesho kutwa kwa maziko mkoani Mara, imefahamika.

Kwa mujibu wa mdogo wa marehemu, Emmanuel Malima, marehemu Cassian ambaye alifariki
dunia juzi katika hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam, ataagwa nyumbani kwake
Savannah, Tabata Mawenzi, kesho kuanzia saa 5 asubuhi.

Alisema baada ya shughuli hizo, mwili huo utapelekwa katika Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Mwalimu J.K. Nyerere, tayari kusafirishwa Jumanne kwenda Musoma, ambako
atazikwa Jumatano.

No comments:

CGP. KATUNGU AWATAKA MAAFISA USTAWI KUELIMISHA WAFUNGWA HAKI NA WAJIBU WAO

  Na. Ssgt Mawazo Mtondo – Dodoma. Mkuu wa Jeshi la Magereza, CGP Jeremiah Yoram Katungu, amewataka Maafisa Ustawi wa Jamii wa Jeshi la Ma...