Sunday, January 11, 2009

Buriani Casian Malima




MWILI wa aliyekuwa Mhariri wa HabariLeo, Cassian Malima (44) utaagwa kesho na
kusafirishwa kesho kutwa kwa maziko mkoani Mara, imefahamika.

Kwa mujibu wa mdogo wa marehemu, Emmanuel Malima, marehemu Cassian ambaye alifariki
dunia juzi katika hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam, ataagwa nyumbani kwake
Savannah, Tabata Mawenzi, kesho kuanzia saa 5 asubuhi.

Alisema baada ya shughuli hizo, mwili huo utapelekwa katika Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Mwalimu J.K. Nyerere, tayari kusafirishwa Jumanne kwenda Musoma, ambako
atazikwa Jumatano.

No comments:

RAIS DKT.MWINYI AKAGUA MRADI WA MJI WA AFCON FUMBA, AANGALIA MAENDELEO YA UWANJA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Hussein Ali Mwinyi , leo Aprili 14, 2026, ameandika historia mpya baada ya kukagua ma...