Saturday, February 21, 2026

WAZIRI MKUU KUANZA ZIARA YA KIKAZI MKOANI ARUSHA FEBUARI 22 -24, 2026

 


Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu ujio huo wa Waziri Mkuu mkoani Arusha 

Na Happy Lazaro,Arusha .

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba anatarajiwa kuwa na ziara ya Kikazi Mkoani Arusha kuanzia Februari 22-24, 2026, akitarajiwa kutembelea na kukagua miradi sita yenye thamani ya shilingi Bilioni 194.2 kwenye Wilaya za Arumeru, Arusha na Longido pamoja na kuzungumza na wananchi. 

Akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake leo Jumamosi Februari 21, 2026, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla amesema Waziri Mkuu kesho Jumapili ataweka jiwe la msingi kwenye mradi wa ujenzi wa bweni la kisasa la Chuo kikuu cha Kimataifa cha sayansi cha Nelson Mandela, kukagua upanuzi wa Miundombinu ya Hospitali ya Oltrumet pamoja na kuzungumza na wananchi eneo la Ngaramtoni. 

“Tarehe 23, Mhe. Waziri Mkuu atakuwa Wilaya ya Longido na atatembelea na kupokea taarifa ya mradi mkubwa wa maji Kata ya Sinya, atazindua mradi wa upanuzi wa shule ya Sekondari Sinya iliyopanuliwa na kuwa na Kidato cha tano na sita na baadae kutembelea kituo cha utoaji wa huduma za Pamoja (One stop Border Post), Namanga na kisha kuzungumza na wananchi kwenye Viwanja vya shule ya msingi Namanga.” 

amesema CPA Makalla. 

Aidha CPA Makalla amewaalika wananchi wote kushiriki katika ziara hiyo, na kusema kuwa kwa siku ya tatu Mhe. Waziri Mkuu atafanya ziara yake Wilaya ya Arusha akitarajiwa kukagua maendeleo ya ujenzi wa kituo Kikuu cha mabasi Jiji la Arusha eneo la Bondeni City, kuweka jiwe la msingi kwenye ujenzi wa soko la Kilombero pamoja na kuzungumza na wananchi kupitia mkutano wa hadhara kwenye eneo hilo la soko Jijini Arusha.



No comments:

DKT.JAFO AWEZESHA ELIMU YA UFUNDI, AKABIDHI VYEREHANI VINNE CHUO CHA FDC KISARAWE-MZENGA

  Taasisi ya Jafo Education Foundation imefadhili jumla ya vijana 51 kusoma katika Chuo cha FDC Kisarawe – Mzenga, kwa lengo la kuwawezesh...